• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:33 AM
Kuhangaisha Miguna ni njama ya kuvuruga muafaka wa Uhuru na Raila, asema mbunge

Kuhangaisha Miguna ni njama ya kuvuruga muafaka wa Uhuru na Raila, asema mbunge

Na CHARLES WASONGA
MBUNGE wa Nyando Jared Opiyo amedai kuzuiliwa na kuhangaishwa kwa mwanaharakati wa vuguvugu la “National Resistance Movement” (NRM) kunachochewa kwa viongozi fulani ambao wangependa kuvuruga matunda ya mwafaka kati ya Rais Uhuru Kenyatta na kiongozi wa NASA Raila Odinga.
Bila kuwataja majina, mbunge wa huyo chama cha ODM alisema viongozi hao aliosema wanatoka mrengo wa Jubilee hawajafurahishwa na hatua ya viongozi hao wawili kushirikiano kwa lengo la kuleta maridhiano ya kisiasa humu nchini.
“Kama Mbunge wa Nyando anakotoka Bw Miguna Miguna naamini kuwa walioamuru Miguna azuiliwe kuingia humu kulingana na agizo la mahakama walenga kuvuruga manufaa ya muafaka kati ya Rais Kenyatta na Raila Odinga.
Ilikuwa aibu kubwa kwa maafisa wa polisi kumdhulumu Bw Miguna mbele ya Bw Odinga kwa saa nyingi katika uwanja wa ndege,” Bw Okello akasema alipowahutubia wanahabari Jumanne alasiri katika majengo ya Bunge, Nairobi.
Bw Okello alisema atawasilisha kesi mahakamani kutaka Bw Miguna aachiliwe huru kutoka uwanjia wa JKIA ambako amekuwa akizuliwa kwa zaidi ya saa 20 baada ya kuwasili nchini kutoka Canada.
Kuzuiliwa kwa Bw Miguna kuliibua makabiliano makali katika uwanja wa huo pale maafisa wa usalama walipojaribu kumsafirisha kwa ndege hadi Dubai lakini akadinda huku akipiga mayowe uwanjani humo hali iliyopelekea rubani wa ndege kuamuru aondolewe.

You can share this post!

Bila Miguna, hakuna amani, wakazi Kisumu waimba

Mtoto aliyejitwika jukumu la kumlea mamaye mlemavu

adminleo