• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 6:50 PM
NTV huru kupeperusha kipindi korti ikitupilia mbali kesi

NTV huru kupeperusha kipindi korti ikitupilia mbali kesi

Na Sam Kiplagat

MAHAKAMA moja Nairobi imefutilia mbali kesi ambapo Shirika la kupigania Maslahi ya Watoto Nchini (CWS) lililenga kuizuia NTV dhidi ya kupeperusha kipindi kinachofichua maovu yanayotendeka katika taasisi hiyo ya umma.

CWS ilikuwa imefika katika korti ya watoto na kupata amri ya kuzuia upeperushwaji wa kipindi hicho.

Kampuni ya Nation Media Group ilitii amri na kusitisha upeperushaji wa kipindi hicho baada ya kukabidhiwa agizo la mahakama.

Kupitia mawakili wake wakiongozwa na Bw Gitonga Mureithi, NMG iliwasilisha kesi ikitaka kutupiliwa mbali kwa kesi hiyo ikihoji kuwa mahakama ya watoto ni korti maalum na inajishughulisha tu na masuala ya watoto wala si kuchafuliwa jina.

Kulingana na Bw Mureithi, kesi ya CWS ililenga kutetea sifa yake na haikuwa na lolote kuhusu maslahi ya watoto.

Korti ilisisitiza kuwa CWS ilikuwa ikidai fidia katika kesi hiyo na haikuwa na mamlaka ya kuendelea kusikiza.Hakimu alitoa uamuzi kuwa hakukuwa na uhusiano kati ya kesi hiyo na ulinzi wa watoto kwa sababu kesi hiyo ilidai fidia kwa kuchafuliwa jina.

 

You can share this post!

Kikao cha Raila na Jumwa chazua mihemko mitandaoni

Amerika yalalama madaktari wa Cuba wanateswa

adminleo