• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
Jeraha lapona, Cherop sasa kushiriki mbio za Rome Marathon

Jeraha lapona, Cherop sasa kushiriki mbio za Rome Marathon

Na GEOFFREY ANENE

MALKIA wa Boston Marathon mwaka 2012, Sharon Cherop ameingia mbio za Rome Marathon nchini Italia mnamo Aprili 8, 2018.

Cherop, 34, ambaye amekuwa akisumbuliwa na jeraha la goti, ni miongoni mwa wakimbiaji 14, 100 waliothibitisha kushiriki katika makala haya ya 34. Aliambia shirika la habari la Xinhua kwamba yuko tayari kufufua taaluma yake mjini Rome.

“Nahisi niko katika hali nzuri baada ya kupitia wakati mgumu kwa muda. Hata hivyo, nafahamu haitakuwa rahisi kushindana na majina makubwa,” alisema Machi 28.

Cherop, ambaye muda wake bora katika mbio hizi za kilomita 42 ni saa 2:22:28 kutoka Berlin Marathon nchini Ujerumani mwaka 2013, atakabiliana na bingwa wa mwaka 2016 na 2017 Muethiopia Rahma Tusa (2:25:12).

Wakenya wengine wanaopigiwa upatu kufanya vyema mjini Rome ni Angela Tanui (2:26:31) na Jafred Chirchir Kipchumba (2:05:48).

Mwaka 2017, Ethiopia ilifagia mataji ya wanaume na wanawake kupitia Shura Kitata na Tusa, mtawalia.

Amos Kipruto na Helena Kirop wanasalia Wakenya wa mwisho kushinda mataji ya Rome Marathon walipotawazwa mabingwa mwaka 2016 na 2013, mtawalia.

You can share this post!

Mathare kuchupa juu ya Gor wakiilima Chemelil Sugar

Gor yakanusha kutowalipa wachezaji licha ya kutatizika...

adminleo