• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 4:31 PM
KRU yatangaza kikosi cha wachezaji 35 wa Simbas 2018

KRU yatangaza kikosi cha wachezaji 35 wa Simbas 2018

Na GEOFFREY ANENE

SHIRIKISHO la Raga la Kenya (KRU) limetangaza kikosi cha wachezaji 35 kitakachowakilisha Kenya kimataifa kwenye raga ya wachezaji 15 kila upande mwaka 2018 likiwemo Kombe la Afrika.

Kuna wachezaji saba wapya kabisa kikosini ambao ni Coleman Were, Patrick Ouko, Peter Waitere, Michael Wanjala, Mohamed Omolo, Johnstone Mung’au na Aggrey Kitoi. Wachezaji Joseph Odero na Levy Amunga wamerejea katika kikosi cha mazoezi.

Amunga, ambaye alishiriki mashindano ya raga ya wachezaji saba kila upande ya Victoria Falls nchini Zimbabwe mnamo Machi 24-25, alikuwa muhimu katika kampeni ya Blak Blad ya Chuo Kikuu cha Kenyatta kumaliza Ligi Kuu ya msimu 2017-2018 katika nafasi ya 10. Kitoi ndiye mchezaji wa pekee kikosini ambaye hayuko kwenye Ligi Kuu.

Alishiriki Ligi Kuu ya msimu 2017-2018, lakini timu yake ya Kisii iliteremshwa daraja baada ya kumaliza ndani ya mduara hatari wa kutemwa.

Kikosi hiki kitanolewa na kocha mpya kutoka New Zealand, Ian Snook, ambaye anatarajiwa kuingia Kenya wakati wowote mwezi wa Aprili. Snook alichukua nafasi ya raia wa Afrika Kusini, Jerome Paarwater, ambaye alitimuliwa Desemba mwaka 2017.

Kombe la Afrika litatumika kama shindano la kufuzu kushiriki Kombe la Dunia mwaka 2019.

KIKOSI CHA KENYA SIMBAS

Washambuliaji:

KCB – Moses Amusala, Oscar Simiyu, Curtis Lilako, Peter Karia, Oliver Mang’eni, Davis Chenge, Martin Owila, Peter Waitere

Kabras Sugar – Joseph Odero, Coleman Were, George Nyambua

Impala Saracens – Dennis Karani, Eric Kerre

Homeboyz – Patrick Ouko, Philip Ikambili, Steve Otieno

Kenya Harlequins – Wilson K’Opondo (nahodha)

Decazevillois (Ufaransa) – Simon Muniafu

Strathmore Leos – Elkeans Musonye

Mabeki:

Impala Saracens – Samson Onsomu, Nato Simiyu, Leo Seje, Vincent Mose

KCB – Michael Wanjala, Jacob Ojee, Peter Kilonzo, Darwin Mukidza

Homeboyz – Mohamed Omollo, Tony Onyango

Blak Blad – Levy Amunga

Nondescripts – Biko Adema

Kenya Harlequins – Dennis Muhanji

Mwamba – Brad Owako

Kabras Sugar – Johnstone Mung’au

Kisii – Aggrey Kitoi

Ratiba ya Simbas ya Kombe la Afrika (2018):

Juni 23 – Morocco vs. Kenya (ugenini)

Juni 30 – Kenya vs. Zimbabwe (nyumbani)

Julai 7 – Kenya vs. Uganda (nyumbani)

Agosti 11 – Kenya vs. Tunisia (nyumbani)

Agosti 18 – Namibia vs. Kenya (ugenini)

You can share this post!

Demu ashtua walevi kulilia kileo kilabuni

SHAIRI: Serikali tunaomba, muwalipe wahadhiri

adminleo