• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 5:55 AM
Kauli za watoto kuhusu Krismasi

Kauli za watoto kuhusu Krismasi

Mwanahabari wetu Sammy Kimatu alitangamana na wanafunzi wa  Amazing Grace Academy, Kaiyaba, Kaunti ya Nairobi kuhusu uelewa wao wa Sikukuu ya Krismasi.

Swali: Naomba unipe hoja yako kuhusu jinsi unavyoielewa Sikukuu ya Krismasi

Fridah Nzisa, 10 (pichani juu)

Siku hii ni kubwa kwangu kwa sababu ndiyo Mwokozi Yesu Kristo alizaliwa ili anifilie kwa ajili ya dhambi zangu.

Caroline Mugambi. Picha/ Sammy Kimatu

Caroline Mugambi, 11

Huku Bwana Yesu anaposherehekewa kuzaliwa kote duniani, wazazi huwa wanawapamba wanao kwa mavazi mapya.

Shantel Mwikali. Picha/ Sammy Kimatu

Shantel Mwikali, 10

Ni siku kubwa kwa familia kupeleka watoto nje kutembea na kubarizi na pia kwenda kanisani kwa maombi.

Winnie Ndinda. Picha/ Sammy Kimatu

Winnie Ndinda, 10

Licha ya wanaopinga na kubishania tarehe kamili ya Yesu kuzaliwa, naamini muhimu ni kuwa alizaliwa kuokoa wanadamu.

Eunice Njeri. Picha/ Sammy Kimatu

Eunice Njeri, 8

Ni kukumbuka Yesu wetu alipozaliwa Bethelemu, nchi ya Juda wakati wa enzi ya mfalme Herodi kutawala.

Mercy Wambui. Picha/ Sammy Kimatu

Mercy Wambui, 7

Ni siku kubwa ulimwenguni kuona watoto walifurahia nguo mpya na kupikiwa vyakula pamoja na kutangamana na wageni.

Kelvin Mutuku. Picha/ Sammy Kimatu

Kelvin Mutuku, 10

Krismasi ni siku kunapowekwa baluni na maua nyumbani na maeneo ya burudani kuashiria ukubwa wake.

Prince Kilunda. Picha/ Sammy Kimatu

Prince Kilunda, 8

Ni siku ya nyimbo, kupamba miti kwa maua huku mifugo kama vile kuku, mbuzi na ng’ombe wakiwa vitoweo kwa binadamu.

Evans Mutambu. Picha/ Sammy Kimatu

Evans Mutambu, 10

Licha ya wakristo kuiweka kama ukumbusho wa kuzaliwa kwa Yesu, inatakiwa sisi kuwakumbuka wasiobahatika katika jamii.

Reagan Machuki. Picha/ Sammy Kimatu

Reagan Machuki, 7

Ni siku ambayo wakristo huamini Yesu alifariki na kufufuka tena kwa ajili ya dhambi zao.

Joseph Mburu. Picha/ Sammy Kimatu

Joseph Mburu, 12

Ni siku yenye mbwembwe zake kuanzia jumbe za kutakiana mema na baraka zake Rabuka.

James Mutemi. Picha/ Sammy Kimatu

James Mutemi, 9

Kila kalenda huandikwa Disemba 25 kwa wino mwekundu kumaanisha Mkombozi alizaliwa kama binadamu duniani.

You can share this post!

Wakenya washauriwa kutumia baiskeli kama njia mbadala ya...

Seneta Samson Cherargei akamatwa kuhojiwa DCI

adminleo