• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 8:27 PM
Marufuku kwa wabunge wa Ruto kuhutubu kanisani

Marufuku kwa wabunge wa Ruto kuhutubu kanisani

NA MWANDISHI WETU

WABUNGE 10 wanaoegemea upande wa Naibu Rais William Ruto, Jumapili walikatazwa kuhutubu katika Kanisa Anglikana la St Thomas, Kerugoya, Kaunti ya Kirinyaga.

Wabunge hao wa mrengo wa Tangatanga walikuwa wameandamana na Dkt Ruto kwa ibada, lakini Mbunge Mwakilishi wa Wanawake wa Kaunti ya Kirinyaga, Bi Wangui Ngirici pekee ndiye alikubaliwa kuhutubu kando na Naibu Rais.

Hatua hiyo ilitokana na agizo la Askofu Mkuu wa ACK, Jackson ole Sapit kwamba siasa zisiruhusiwe kanisani. Bi Wangui alikubaliwa kuwataja wanasiasa waliokuwepo.

Wakati Dkt Ruto alipohutubu, alihakikishia wasimamizi wa kanisa kwamba watafuata maagizo yao.

‘Tunaheshimu kanisa na hatutaingiza siasa zozote,’ akasema. Baadhi ya wabunge waliokuwepo ni Munene Wambugu (Kirinyaga Central), Gichimu Githinji (Gichugu), Ndindi Nyoro (Kiharu) na Alice Wahome (Kandara).

Naibu Rais alitoa wito kwa wanasiasa wote nchini kuweka tofauti zao kando ili wamsaidie Rais Uhuru Kenyatta kutekeleza ajenda zake za maendeleo.

Na George Munene

Wakati huo huo, alitoa wito kwa Wakenya kuombea familia ya Rais Mstaafu Daniel arap Moi aliyefariki Jumanne iliyopita.

You can share this post!

Moi atakavyozikwa kwa heshima ya kipekee

Wachezaji densi waliomtumbuiza Moi wadai Kibaki aliwadharau

adminleo