• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 5:46 PM
Wabunge wa Kenya kuchuana na wenzao kutoka Uturuki

Wabunge wa Kenya kuchuana na wenzao kutoka Uturuki

Na GEOFFREY ANENE

WABUNGE wa Kenya wataweka suti zao kando kwa mechi ya kirafiki dhidi ya wenzao kutoka Uturuki hapo Aprili 17, 2018.

Mchuano huu utasakatwa katika klabu ya michezo ya Parklands jijini Nairobi.

Bunge FC ya Kenya, ambayo imekuwa ikishiriki mashindano ya Afrika Mashariki kwa miaka kadhaa sasa, inatarajiwa kuwakilishwa na wabunge kama Kanini Kega (Kieni), Daniel Wanyama (Webuye West) na Otiende Amollo (Rarieda), miongoni mwa wengine.

Wabunge kutoka Uturuki wamekuwa humu nchini kwa karibu juma moja kufanya mazungumzo jinsi ya kuimarisha uhusiano kati ya mataifa haya katika sekta mbalimbali zikiwemo elimu na biashara.

Mwenyekiti wa Chama cha Kirafiki cha Wabunge kutoka Uturuki na Kenya, Mahmut Kacar anatarajiwa kuongoza timu ya Waturuki.

Spika wa Bunge la kitaifa Justin Muturi atafungua rasmi mchuano huo wa kihistoria saa mbili asubuhi.

You can share this post!

Meneja atetea kampuni kuhusu umiliki wa shamba la Sh8...

Madoya ahakikishia Zoo kuwa itasalia ligini

adminleo