• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 10:08 PM
KRU yasimamisha msimu 2019-2020 kwa sababu ya COVID-19

KRU yasimamisha msimu 2019-2020 kwa sababu ya COVID-19

Na GEOFFREY ANENE

SHIRIKISHO la Raga Kenya (KRU) limesimamisha mashindano yote ya msimu 2019-2020 ikiwemo Ligi Kuu baada ya Wizara ya Afya kuthibitisha Ijumaa kisa cha kwanza cha maakumbizi ya ugonjwa wa COVID-19 unaosababishwa na virusi vya corona.

“Kufuatia tangazo kuwa kuna mtu anaugua ugonjwa wa COVID-19 humu nchini na pia agizo la Wizara ya Afya kupiga marufuku mikusanyiko ya watu, KRU inatangaza kusitisha msimu wa 2019-2020.

Marufuku haya yataanza kutumikiwa katika mechi za Ligi Kuu, Ligi ya Daraja la Pili, Ligi ya Matawi na Eric Shirley Shield za wikendi hii,” shirikisho limesema na kuahidi kutoa mwelekeo zaidi baadaye.

Mechi za Ligi Kuu zilizokuwa zimeratibiwa kusakatwa Machi 14 ni kati ya Homeboyz na Menengai Oilers na ile inayokutanisha Impala Saracens na Stanbic Mwamba uwanjani Impala Club.

Mechi hizo ni za kuamua timu mbili zitakazomenyana na Kabras Sugar na mabingwa watetezi KCB katika nusu-fainali.

You can share this post!

AFYA: Faida za kiafya kuyala machungwa

Familia yalilia haki ya mtoto wao aliyegongwa na gari

adminleo