• Nairobi
  • Last Updated April 16th, 2024 6:55 PM
CORONA: Daktari motoni kwa kukataa kuhudumia wagonjwa

CORONA: Daktari motoni kwa kukataa kuhudumia wagonjwa

NA RUTH MBULA NA FAUSTINE NGILA

DAKTARI mmoja katika Hospitali ya Mafunzo na Rufaa ya Kisii (KTRH) yuko taabani na huenda atapigwa kalamu baada ya kudinda kuwahudumia wagonjwa, akitaja ukosefu wa maandalizi kutokana na virusi vya corona. 

Hospitali hiyo ambayo ndiyo kubwa zaidi katika eneo la Nyanza Kusini, sasa inapanga kumchukulia hatua za kinidhamu ambazo zinalenga kumtimuakazini daktari huyo.

Katika barua iliyoonekana na Taifa Leo Dijitali, afisa mkuu mtendaji wa hospitali hiyo Emock Ondari alisema kitendo cha daktari huyo kilionyesha utovu wa nidhamu ya kitaaluma, na anafaa kuadhibiwa.

“Hata hivyo, kabla ya hatua yoyote kuchukuliwa, umeitwa kuelezea ni kwa nini adhabu dhidi yako haifai kufanyika,

“Wanakuwakilisha, iwapo wapo, wanafaa kufika katika ofisi hii kabla ya saa 72 kutoka siku ya kuandikwa kwa barua hii, ukikosa basi hatua iliyopangwa itachukuliwa dhidi yako bila hata kushirikishwa,” barua hiyo ilisema.

Inadaiwa daktari huyo alikataa kuwashughulikiwa wagonjwa waliotaka kutibiwa hospitalini humo licha ya kuagizwa na mkuu wa huduma za matibabu na Bw Ondari.

“Ulidai hakuna barakoa za N95 licha ya kupewa barakoa za upasuaji, maji na sabuni.”

You can share this post!

Kafyu hii iondolewe – LSK

Mawakili wataka korti zifunguliwe mrundiko wa kesi upungue

adminleo