• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 9:40 PM
Polo aona moto kuchezea maski

Polo aona moto kuchezea maski

NA MARU WANGARI

LIMURU MJINI

JAMAA mjini hapa alijipata mashakani kwa kufanyia utani masharti ya kujikinga na corona.

Yote yalianza kalameni huyo alipojipaka rangi nyeupe usoni kuwatania maafisa wa usalama kuwa alikuwa amevalia maski.

Polo huyo ajichora rangi hiyo kuanzia kwenye pua lake, midomoni mashavuni na hadi kwenye masikio yake kwa namna iliyofanya aonekana alikuwa amevalia maski.

Wakazi hawakuamini macho yao walipogundua polo huyo alikuwa amejichora ionekane amevalia maski huku akiendelea na shughuli zake kama kawaida na kutangamana na watu sokoni.

Baadhi walikashifu kitendo cha jamaa huyo huku wakisema alikuwa akihatarisha sio tu maisha yake, bali pia maisha ya wakazi kwa kufanyia utani maagizo yaliyotolewa na serikali kuhusu kujikinga na maambukizi ya virusi vya corona.

Hata hivyo, jombi huyo alijipata mashakani alipokutana na maafisa wa polisi waliokuwa wakipiga doria mjini humo.

Baada ya polo huyo kufahamu kwamba utukutu wake ulikuwa umegunduliwa na maafisa hao, alichana mbuga kuwakwepa polisi ambao walimfuata unyo unyo na kumkamata.Kulingana na mdokezi wetu, kalameni huyo, alijitetea kwa polisi akisema aliamua kufanya hivyo kwa kukosa hela za kununua maski.

‘Maski zinauzwa Sh50 na sina uwezo wa kununua kwa sababu sijakuwa nikifanya kazi sasa kwa karibu mwezi mmoja tangu tuliposimamishwa. Nilitafuta mbinu za kusaka chakula na wakati huo huo kuepuka kukamatwa kwa kutokuwa na maski ndipo wazo hilo liliponijia,’ alijitetea akiwaomba polisi kumwachilia.

Juhudi zake za kujitetea ziliambulia patupu huku polisi wakimburura na kumweka katika gari lao akisubiri adhabu kisheria.

Na Mary Wangari

You can share this post!

ODONGO: Polisi wakome kutumia Covid-19 kuendeleza ufisadi

Kwaheri Walibora, wengi tutakupeza

adminleo