• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 10:50 AM
MALEZI NA LISHE: Aina za vyakula unavyoweza kumpa mtoto mchanga

MALEZI NA LISHE: Aina za vyakula unavyoweza kumpa mtoto mchanga

Na MARGARET MAINA

[email protected]

KWA miezi sita ya kwanza punde mtoto anapokuwa amezaliwa, huwa anatosheka na maziwa ya mama kwa lishe au hata wakati mwingine maziwa ya kopo kwa wale wasionyonyeshwa.

Lakini baada ya muda wa miezi sita na kuendelea, mtoto anahitaji vyakula aina aina na si tu maziwa.

Ni hapo ndipo unatakiwa umpatie chakula zaidi. Lakini kwa mama ambaye ndiye kwanza analea kwa mara ya kwanza, ni kipindi kigumu kwani yumkini hajui ni chakula gani cha kumpa mwanawe.

Ukiwa wewe ni mama mzazoLazima umpatie vyakula vyenye lishe bora.

Vyakula vyenye madini ya chuma

Vyakula hivi ni muhimu sana katika ukuaji wa mtoto, madini ya chuma husaidia uzalishwaji wa haemoglobin, vilevile madini ya chuma yanasaidia ukuaji wa ubongo wa mtoto.

Vyakula hivyo ni kama, nyama ya ngombe,kuku, samaki,mayai ,parachichi na spinach.

Vyakula vyenye madini ya zinki

Vyakula vilivyo na zinki pia husaidia ubongo wa mtoto ukue vizuri na haraka. Zinki inasaidia seli za mwili kukua na kujiimarisha zenyewe kupambana na magonjwa. Vyakula hivi ni kama nyama, kuku, na samaki.

Vyakula vya madini ya Calcium na Vitamini D

Calcium ni muhimu kwa kuwa na mifupa imara, na vitamini D husaidia na ni muhimu pia. Madini haya yako kwenye maziwa lakini kwa kiasi kidogo unaweza kuyapata kwenye peanut, mtindi, mayai, na samaki.

Vyakula vyenye Omega 3 / DHA

Kwa watu wazima, Omega 3 imesaidia sana hasa kwa wenye ugonjwa wa moyo. Vilevile kwa watoto ina faida kama hizo. Kwa mtoto wa umri mdogo husaidia kwa kiasi kikubwa katika upande wa yeye kuwa na ubongo wenye afya na macho yenye kuona vizuri. Vyakula vilivyo na Omega 3 ya kutosha ni samaki aina ya salmon, na parachichi.

Vyakula vyenye Vitamini A, B, C na E

Hizi aina nne za vitamini huusaidia mwili kwa kuweza kuwa na ubongo wenye afya, kuwa na macho yanayoona vizuri, na ngozi inayong’aa vizuri. Hupatikana kwa vyakula kama karoti, viazi vitamu (hivi vina kiwango kikubwa cha vitamini A). Mboga za majani ya kijani, ndizi, na maharage husheheni vitamini B, nyanya zina Vitamini C, na mahindi, na mchele huwa na vitamini E kwa kiwango kikubwa.

You can share this post!

SIHA NA LISHE: Umuhimu wa kula saladi

MAPISHI NA UOKAJI: Jinsi ya kupika mkate tambarare uitwao...

adminleo