• Nairobi
  • Last Updated March 19th, 2024 1:13 PM
LISHE: Biryani na nyama ya mbuzi

LISHE: Biryani na nyama ya mbuzi

Na MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 20

Mapishi: Dakika 40

Walaji: 3

Vinavyohitajika

  • kilo nusu mchele wa Basmati
  • kilo 1 nyama ya mbuzi kata katika umbo dogo kisha ichemshe na tangawizi, kitunguu saumu, unga wa binzari, pilipili na chumvi.
  • vitunguu maji 4
  • nyanya 6 iliyokatwakatwa
  • mafuta ya kupikia
  • kijiko 1 kidogo cha pilipili
  • kijiko ½ unga wa binzari
  • vijiko 3 vyaungawagiligilani
  • vijiko 2 vyamchanganyikowatangawizinakitunguuswaumuvilivyosagwa
  • mbegu 10 za hiliki
  • majani ya bay 4
  • majani ya mint
  • chumvi
Biryani na nyama ya mbuzi huwa chakula chenye ladha. Picha/ Margaret Maina

Maelekezo

Weka mafuta katika sufuria yapate moto, kisha kaanga nyama yako iliyokwishachemshwa mpaka iwe na rangi ya kahawia.

Kisha itoe nyama hiyo na ichuje mafuta na mafuta yanayobaki weka kitunguu na uendelee kukaanga kwa dakika 10. Sasa weka binzari, pili pili, giligilani, bay leaves na mbegu za hiliki.

Changanya vizuri upate mchanganyiko mzuri mkavu; mwagilia yale maji uliyotunza baada ya kuchemshia ile nyama.

Kisha weka nyanya ndani ya sufuria yako; pika mpaka maji yakauke na mafuta yaanze kuonekana kwa juu ndani ya sufuria.

Kisha weka nyama yako ndani ya sufuria halafu punguza moto. Acha ijipike kwa muda mpaka mchuzi wako na nyama viwe na ladha. Pia usisahau kuweka chumvi kulingana na ladha unayopenda.

Chukua sufuria nyingine weka mafuta ya kupikia na vitunguu kisha kaanga na majani ya giligilani, majani ya mint na korosho kisha funika kwa dakika 10.

Weka mchele wako mkavu uliokwishaoshwa vizuri na uchanganye vizuri. Ongeza vikombe vitano vya maji na chumvi kidogo.

Mchele ukishaanza kuchemka, funika sufuria na punguza moto.

Maji yakisha kauka kiasi, weka mchanganyiko wa ile nyama yako nusu tu juu ya wali wa Basmati na acha wali uive kabisa. Sasa utakua tayari kupakua na kula chakula chako.

Pakua na ufurahie.

You can share this post!

Maseneta wataka kubuniwe afisi ya kushughulikia usalama wao

TUNAWEZA: Mtindio wa ubongo haukuzima ndoto yake