• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
MAPISHI NA UOKAJI: Jinsi ya kupika mkate tambarare uitwao naan

MAPISHI NA UOKAJI: Jinsi ya kupika mkate tambarare uitwao naan

Na MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaa: Saa moja

Muda wa mapishi: Dakika 30

Walaji: 5

Vinavyohitajika

• unga wa ngano gramu 500

• kijiko kidogo cha hamira

• maji fufutende kikombe 1

• kijiko 1 cha chai cha chumvi

• kijiko 1 cha sukari

• kijiko kikubwa cha siagi

Unga uliokandwa. Picha/ Margaret Maina

Maelekezo

Changanya katika bakuli hamira, maji fufutende na sukari kisha koroga mpaka hamira iyeyuke kabisa. Ukisha fanya hivyo, weka kando kwa muda wa dakika tano.

Weka unga wa ngano, chumvi na uchanganye vizuri.

Mwagia yale maji yenye mchanganyiko wa hamira na uanze kukanda vizuri unga wako. Hakikisha umeshikana na ni laini au mwororo.

Baada ya kukanda, funika bakuli lako kwa taulo ya jikoni kisha weka sehemu yenye joto la kutosha na acha unga uumuke kwa muda wa saa moja.

Sasa toa mchanganyiko wako wa unga na uanze kuukanda tena kwa dakika tano kabla ya kuanza kugawanisha katika maumbo madogo.

Mwagia unga kiasi juu ya meza kusaidia maumbo hayo yasishike – kukwama – na anza kusukuma kwa kutumia mpini.

Mkate wa naan ukiandaliwa katika kikaangio. Picha/ Margaret Maina

Kisha chukua mkate wako wa Naan, pika bila mafuta halafu paka siagi juu ya mkate wako. Unapoanza kubadilika rangi geuza na paka tena siagi upande wa pili.

Mkate wake huu wa naan ukiiva, epua na pakua na ule huku ukitumia rojo ya mchuzi au supu.

You can share this post!

MALEZI NA LISHE: Aina za vyakula unavyoweza kumpa mtoto...

Duale aponea

adminleo