• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Weta atishia wanaounga mkono kung’olewa kwake

Weta atishia wanaounga mkono kung’olewa kwake

NA SAMWEL OWINO

KUNDI la chama cha Ford Kenya linaloongwza na mbunge wa Kandunyi Wagula Wamunyinyi linalaumu seneta wa Bungoma Moses Wetangula kwa kutishia kamati ya chama hicho.

Bw Wamunyinyi pamoja na katibu wa chama hicho Eseli Simiyu alidai kwamba wanachama hao walikuwa wanalazimisha kukutia saini afidafiti ili kupinga saini zilizochukuliwa ili kumng’oa Bw Wetangula kama kiongozi wa chama wiki iliyopita.

Akiongea kwenye afisi ya msajili wa vyama Nairobi Ijumaa Bw Simiyu alisema kwamba madiwani wateuliwa ambao ni wanachama wa NEC walitishiwa kutolewa.

Wanachama wengine waliambiwa kwamba watatolewa kwenye kamati za kaunti kama hawatabadilisha msimamo wao kuhusu kutolewa kwa Bw Wetang’ula.

“Tutaripoti vitisho hivyo kwa polisi ili wanchama wetu walindwe,” alisema Bw Simiyu..

Lakini mbunge wa Kimini Chris Wamalwa, katibu mkuu aliyeteuliwa na Bw Wetangula, alikana madai hayo. “Si ukweli. Ni uongo mtupu,” Dkt Wamalwa aliambia Taifa Leo.

You can share this post!

Prof Kiama aanza kazi rasmi Chuo Kikuu cha Nairobi

Jamii za mpaka wa Nandi na Kakamega zatakiwa kuishi kwa...

adminleo