• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 2:07 PM
Man City roho mkononi kesi dhidi yao ikianza

Man City roho mkononi kesi dhidi yao ikianza

Na CHRIS ADUNGO

MANCHESTER City wanaanza mojawapo ya wiki ngumu zaidi katika historia yao wakifahamu uwezekano wa hadhi yao kushuka, ndoto za kujinyakulia ufalme wa Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) kuvurugwa na kusambaratika kabisa kwa kikosi chao.

Hii ni kufuatia mwanzo wa kesi ya rufaa dhidi ya marufuku ya kusalia nje ya kipute cha UEFA kwa kipindi cha miaka miwili ijayo. Kesi hiyo itasikilizwa na Jopo la Mizozo ya Spoti Duniani (CAS) kuanzia Juni 8, 2020.

Mnamo Februari 14, 2020, Kitengo cha Uefa cha kudhibiti matumizi ya fedha miongoni mwa klabu za bara Ulaya (CFCB) kilipiga Man-City faini ya Sh3.5 bilioni baada kupatikana na hatia ya kukiuka sheria za Uefa zinazohusiana na masuala ya matumizi ya fedha na leseni (FFP) kati ya 2012 na 2016.

Kwa upande wao, CFCB pia walishikilia kwamba Man-City walikosa kushirikiana vilivyo na vinara wa vitengo vya Uefa waliokuwa wakiichunguza keshi hiyo dhidi yao.

Pindi baada ya kutolewa kwa marufuku hayo, Man-City walikata rufaa kusisitiza kwamba CFCB haikuendesha uchunguzi wake kwa haki kwa sababu nyingi za habari zilizotegemewa na idara hiyo hazikutolewa na klabu. Chini ya kocha Pep Guardiola, Man-City wana imani tele kwamba watafaulu katika kesi yao itakayosikiliwa na majaji watatu wa CAS kwenye vikao vya siku tatu vitakavyoendeshwa kwa njia ya video.

Maamuzi ya jopo la CAS yatafichuliwa mwishoni mwa msimu huu. Iwapo CAS itadumisha marufuku ya Man-City, basi kikosi hicho hakitashiriki kampeni za UEFA msimu ujao na hawatanogesha kivumbi cha Super Cup mwanzoni mwa muhula ujao hata kama wataibuka washindi wa taji la UEFA msimu huu.

Rais wa La Liga ameshikilia kwamba Man-City wanastahili kuadhibiwa vikali kwa sababu kwa pamoja na Paris Saint-Germain (PSG) nchini Ufaransa, wamekuwa wakishiriki ulaghai kwa kukiuka kanuni za FFP.

You can share this post!

Eastleigh yaamka tena kibiashara baada ya majuma kadhaa ya...

Jinsi ya kupika spring rolls

adminleo