• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
TAHARIRI: Pendekezo la vyuo laonyesha ubinafsi

TAHARIRI: Pendekezo la vyuo laonyesha ubinafsi

NA MHARIRI

MJADALA kuhusu kurejelea masomo kabla ya Januari mwaka huu, unaibua maswali mazito kuhusu wadau wa sekta ya kibinafsi.

Wamiliki wa shule za Kibinafsi pamoja na vyuo, wamemlaumu Waziri wa Elimu, Profesa Gerorge Magoha kwa kutangaza kwamba hakuna taasisi yoyote ya elimu itakayofunguliwa mwaka huu.

Awali, waziri alikuwa amesema huenda vyuo vingelifunguliwa Septemba.Lakini alipokuw aakibadili msimamo huo, alisema baada ya ukaguzi, ilikuwa wazi kuwa ni vyuo vichache ambavyo vilikuwa vimetimiza masharti ya kukabili maambukizi ya Corona.Chama cha Vyuo Binafsi (Kapco) kinasema vyuo vingi vina viwanja na majengo yanayoweza kuwa na wanafunzi wengi bila ya kuvunja kanuni hizo.

Nao wale wa chama cha shule za kibinafsi (Kepsa), wanasema walimu wengi wanahangaika na baadhi wamejiua kwa kukosa mishahara ya miezi kadhaa.

Kwa hivyo, wasimamizi wa taasisi hizo wanasema ingekuwa vyema kama serikali itawaruhusu wamiliki shule na vyuo vya kibinafsi kuendelea na masomo kuanzia Septemba.Maombi hayo yanaonekana kuwa yanayotolewa bila ya kuzingatia uhalisia wa mambo.

Vyuo na shule za kibinafsi husomesha watoto wa Wakenya, ambao wengi wao wameathirika kiuchumi tangu janga la Corona litokee.Mzazi aliye na mtoto katika shule au chuo cha kibinafsi, ni Mkenya ambaye anajali afya ya mwanawe sawa na yule aliye na mtoto katika shule ya umma.

Kumwambia amwache mwanawe wa shule ya umma nyumbani kisha yule aliye shule ya kibinafsi asome, ni ubaguzi. Mfumo wa elimu nchini haujabagua kwamba kuna elimu ya wanafunzi wa taasisi za kibinafsi na mwingine wa zile za umma. Pili, itaonyesha kuwa hajali afya ya mwanawe bali masomo.

Elimu haina mwisho, mtu anaweza kusoma wakati wowote, bora kuna uhai na hali inaruhusu kufanya hivyo. Kama uchunguzi uliofanywa na serikali unaonyesha kwamba mijengo mingi inaendelea kutumika kama vituo vya kuzuilia watu wanaoshukiwa kuambukizwa virusi vya Covid-19.

Kuiharakisha serikali iruhusu watu wa taasisi za kibinafsi kuendelea na masomo wakati kama huu, kunaonyesha wahusika wanasahau kwamba elimu inahusisha watoto, ambao takwimu za hivi punde zinaonyesha hata wao wako katika hatari ya kuuawa na Corona.

You can share this post!

Fyata ulimi, Uhuru amuonya Kang’ata

Madaktari washinikiza kupewa bima ya afya

adminleo