• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 5:55 AM
Wawili wajeruhiwa baada ya V8 kugonga nguzo za barabarani

Wawili wajeruhiwa baada ya V8 kugonga nguzo za barabarani

Na SAMMY WAWERU

WATU wawili Jumanne wamenusurika kifo baada ya gari walimokuwa kupoteza mwelekeo na kugonga chuma katika barabara kuu ya Thika Superhighway.

Ajali hiyo ilitokea eneo la Carwash, kati ya mtaa wa Githurai na Kasarani.

Kulingana na walioshuhudia, gari hilo aina ya V8 lilikuwa likiendeshwa kwa mwendo wa kasi.

“Lilikuwa kwa mwendo wa kasi sana, na tuligutushwa na kishindo cha kugonga chuma kilichoko kandokando mwa barabara ya kasi, hadi kikajipinda,” mhudumu mmoja wa bodaboda akaambia Taifa Leo.

Alisema baada ya kugonga chuma, lilielekea katika upande – leni – ya kasi ya juu.

“Ni bahati tu magari yaliyokuwa nyuma yake, yalikuwa mbali,” akasema.

Akithibitisha tukio hilo, mmoja wa maafisa wa trafiki wanaohudumu eneo hilo Fridah Makena, alisema hakukuwa na majeraha.

“Lilikuwa na watu wawili na hakuna aliyejeruhiwa. Hata hivyo, tunaonya watumizi wa Thika Road wawajibike sababu kuendesha gari kwa mwendo wa kasi ni hatari,” akasema.

Visa vingi vya ajali Thika Road vinahusishwa na utepetevu miongoni mwa madereva, uendeshaji wa magari kwa mwendo wa kasi na ubadilishaji wa leni kiholela, hasa katika barabara ya kasi.

Eneo la Carwash, limetajwa kuwa hatari kutokana na ajali za mara kwa mara.

“Eneo hili kila wiki halikosi ajali. Halmashauri ya Barabara Kuu Nchini (KeNHA), itathmini eneo hili,” akapendekeza mmoja wa wenyeji.

Kulingana na mkazi huyo, maafa na majeruhi yameshuhudiwa eneo hilo, licha ya maafisa wa KeNHA kuonekana kupiga doria kila siku.

You can share this post!

Covid-19 imechelewesha azma yangu, haijaifuta –...

Beki Joseph ‘Crouch’ Okumu asema Simba SC hawawezi...

adminleo