• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 5:55 AM
LISHE: Mkate wa ‘tikitimaji’

LISHE: Mkate wa ‘tikitimaji’

Na MISHI GONGO

Idadi ya walaji: 6

Viungo

unga gramu 750

hamira kijiko cha chai 1/4

sukari vijiko vikubwa 3

chumvi kijiko cha chai 1/4

siagi kijiko kimoja kikubwa cha chakula

rangi za nyekundu na kijani

Jinsi ya kutayarisha

Chukua unga wa ngano, hamira, sukari, chumvi, siagi na maji kisha changanya.

Kanda unga wako hadi ulainike kisha ugawanye kwa madonge matatu.

Donge moja tia rangi ya kijani, lingine litie rangi nyekundu na la tatu liwache bila rangi.

Weka pembeni usubiri madonge yako yaumuke.

Unga ukishaumuka sukuma madonge yako uyafanye kuwa kama chapati.

Kisha yakunje yawe umbo la mstatili.

Yaunganishe kwa kuanza na jeupe kuwa ndani, jekundu katikati na kijana nje.

Weka katika mkebe halafu oka kwa dakika 40.

Unaweza kuandaa chakula hiki kwa chai, supu au sharubati.

You can share this post!

Baadhi ya wakazi Mombasa wapinga mpango wa masomo mashinani

VINYWAJI: Jinsi ya kutayarisha sharubati ya karakara na...