• Nairobi
  • Last Updated April 16th, 2024 10:55 AM
Trump aisifu Korea Kaskazini kwa kuharibu kituo cha nyuklia

Trump aisifu Korea Kaskazini kwa kuharibu kituo cha nyuklia

Na MASHIRIKA

Rais wa Amerika Donald Trump Jumamosi alishukuru Korea Kaskazini kwa kukubali kuharibu kituo chake cha kufanyia majaribio silaha za kinyuklia kabla ya mkutano wake na Rais Kim Jong Un nchini Singapore.

“Korea Kaskazini imetangaza kuwa itaharibu kituo chake cha kufanyia majaribio silaha za kinyuklia mwezi huu kabla ya mkutano mkuu Juni 12,” Trump aliandika kwenye Twitter.

“Asante, hiyo ni ishara nzuri sana,” aliongeza.

Kituo hicho kilichoko Punggye-ri, kaskazini mashariki ya Korea Kaskazini kitaharibiwa mbele ya wanahabari wa kigeni kati ya Mei 23 na 25 kama hatua ya Rais Kim Jong Un ya kujitolea kusitisha silaha za kinuklia.

Hata hivyo, kuna wanaodai kwamba nchi hiyo haijatangaza hadharani kujitolea kwake kuachana na silaha zake ikiwa ni pamoja na makombora yaliyo na uwezo wa kufika Amerika.

Amerika inataka Korea Kaskazini iharibu kabisa silaha za kinuklia na ithibitishwe imefanya hivyo na kusisitiza kuwa ni lazima ithibitishwe.

You can share this post!

Morata alishwa kadi ya manjano na mpenziwe, onyo atabaki...

SHANGAZI: Nataka kumsahau mpenzi lakini nalemewa na hisia

adminleo