• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 8:55 PM
Ingwe yawinda mshambuliaji wa Nzoia Sugar

Ingwe yawinda mshambuliaji wa Nzoia Sugar

Na JOHN ASHIHUNDU

KLABU ya AFC Leopards inapanga kuvamia ngome ya Nzoia Sugar kumnasa mshambuliaji matata, Elvis Rupia. Ripoti zimesema shughuli hiyo itafanyika mwezi ujao.

Nyota huyo maarufu kama Machapo, amekuwa muhimu katika kikosi hicho cha kocha Bernard Mwalala ambapo kufikia sasa amefunga mabao 11.

Mbali na Leopards, straika huyo vile vile amevutia timu nyingi zikiwemo za ligi kuu nchini Zambia.

Ingwe vile vile imevutiwa na kiwango cha Pistone Mutamba wa Wazito FC.

Rupia alikuwa mshambuliaji wa Nakuru All Stars kabla ya kuagana nayo iliposhuka ngazi miaka miwili iliyopita.

You can share this post!

Madaktari wa Cuba kutua nchini Mei 28 kuhudumia wagonjwa...

Migne aita wengine wanne kuimarisha kikosi cha Stars

adminleo