• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:50 AM
Kiwanda kipya cha Coca-cola kupunguza ukosefu wa ajira

Kiwanda kipya cha Coca-cola kupunguza ukosefu wa ajira

Na BERNARDINE MUTANU

KAMPUNI ya Coca-Cola imefungua kiwanda cha kutengeneza vinywaji kwa gharama ya Sh7 bilioni katika tawi lake lililoko Embakasi, Nairobi.

Kiwanda hicho kina uwezo wa kutengeneza chupa 28,000 za soda kwa saa moja. Kutokana na hilo, kiwanda hicho kiliunda nafasi 24 za kazi katika tawi hilo.

Tofauti kati ya kiwanda hicho na kiwanda cha kawaida ni kwamba sharubati hupakiwa kwa chupa ikiwa moto sana, alieleza meneja mkurugenzi wa Coca Cola Afrika-Kenya (CCBA) Daryl Wilson.

Ni kiwanda cha pili cha aina hiyo Afrika Mashariki, baada ya kiwanda kingine kama hicho kuzinduliwa Uganda.

Baadhi ya bidhaa zitakazotengenezewa katika kiwando hicho ni sharubati ya matunda, chai iliyotiwa barafu na vinywaji vingine vya spoti.

Kampuni hiyo inapata maembe kutoka Murang’a.

You can share this post!

Wakenya sasa wachangamkia mashangingi

KEBS kuharibu bidhaa za thamani ya Sh250 milioni kwa kukosa...

adminleo