• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:33 AM
LISHE: Jinsi ya kuandaa mkate wa nyama

LISHE: Jinsi ya kuandaa mkate wa nyama

Na MISHI GONGO

Muda wa mapishi: Dakika 40

Viungo

  • unga wa ngano gramu 750
  • hamira kijiko 1/4 cha chai
  • chumvi kijiko cha chai 1/2
  • mafuta ya uto robo kikombe.
  • nyama ya kusaga robo kilo
  • dania vijiti 5
  • boga nusu
  • karoti 1
  • masala kiasi
  • limau kubwa 1

Jinsi ya kutayarisha

Changanya unga wa ngano, hamira, chumvi maji glasi moja, mafuta ndani ya bakuli kisha kanda hadi unga ulainike.

Tengeneza madonge ya kiasi yenye umbo la mviringo kisha weka pembeni yaumuke.

Chukua sufuria, weka nyama, chumvi kisha bandika motoni halafu utie boga, karoti, na dania.

Koroga taratibu hadi nyama yako iive.

Epua kutoka motoni, kisha ikamulie limau na masala. Koroga hadi ichanganyike na viungo.

Chukua madoge yako sukuma kama chapati, mviringo wako uwa na uzito kiasi kisha chukua vijiko vitatu vya nyama uliyoiunga na kumwaga kwenye chapati yako.

Kunja chapati yako mara mbili upate umbo la nusu duara kisha tia kwenye cutter – kifaa cha kukata – iliyo na umbo la nusu duara kisha finyilia.

Ikunje chapati yako mara mbili upate umbo la nusu duara kisha tia kwenye cutter – kifaa cha kukata – iliyo na umbo la nusu duara kisha finyilia. Picha/ Mishi Gongo

Endelea na shughuli hii hadi umalize madonge yako yote. Panga vijikate vyake kwenye trei kisha weka kwenye jiko la kuoka au ovena.

Oka kwa muda wa dakika 40.

Vitoe kwenye jiko au ovena na uache mikate ipoe.

Unaweza ukaandaa mlo huo kwa chai ya tangawizi au sharubati.

You can share this post!

Jinsi ya kuzuia saratani ya matiti

Jinsi ya kulinda afya ya meno ya mtoto