• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 9:55 AM
Makumbi aonyeshwa mlango na Western Stima

Makumbi aonyeshwa mlango na Western Stima

NA CECIL ODONGO

KLABU ya Western Stima ambayo inashiriki ligi ya Supa Jumanne imemwachisha kazi  kocha wake raia wa Uganda Richard Makumbi.

Stima, imekuwa ikisajili matokeo yasiyoridhisha na mnamo Jumapili Julai 22,2018 walibanduliwa nje ya mashindano ya kombe la ngao ya SportPesa na Mabingwa wa KPL mwaka wa 2009, Sofapaka baada ya kulazwa mabao 4-0.

“Kutokana na matokeo mabaya katika mkondo wa pili wa ligi, usimamizi wa klabu umeafikia uamuzi wa kumpiga kalamu Richard Makumbi,” ikasema taarifa kutoka Western Stima FC.

Hili likuwa pigo kubwa kwa wanaumeme hao waliotarajia ushindi na ambao ungewavumisha hadi robo –fainali na kuimarisha uwezo wao wa  kutwaa kombe hilo.

Baada ya kuongoza jedwali la NSL katika mkondo wa kwanza wa ligi, timu hiyo sasa imeshuka hadi nafasi ya pili, alama mbili nyuma ya viongozi Ushuru FC.

Cha kushangaza ni kwamba kikosi cha stima kimeporomoka na kupoteza uongozi hata baada ya kufungua mwanya wa alama 12 kati yao na nambari kabla ya mechi tano za mwisho wa mkondo wa kwanza.

Kufuatia kutimuliwa kwa Makumbi, uongozi wa Western Stima umempokeza usukani kwa muda aliyekuwa naibu kocha wa Kisumu All Stars Paul Ogai.

Makumbi alijiunga na Western Stima Septemba, 2017 kujaza nafasi ya aliyekuwa kocha wa klabu hiyo Henry Omino ambaye pia alionyeshwa mlango kutokana na sababu iyo hiyo ya kusajili matokeo mabaya.

Alitarajiwa kunasua Stima kutoka kwa hatari ya kuteremshwa ngazi ila hakufaulu. Hata hivyo amejizolea sifa kedekede kwa kuleta umoja na udhabiti timuni.

  • Tags

You can share this post!

Kasisi motoni kwa kupora wanawake Sh1.3 milioni

Crested Cranes wapata dawa yao Cecafa

adminleo