• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 5:55 AM
Wakurugenzi 10 kortini kwa kufyonza mamilioni ya KPC

Wakurugenzi 10 kortini kwa kufyonza mamilioni ya KPC

Na RICHARD MUNGUTI

WAKURUGENZI  kumi  kutoka kampuni mbalimbali walishtakiwa Jumatatu kwa kupokea kwa njia za ufisadi Sh15milioni kutoka kwa  kampuni ya usambazaji nguvu za umeme nchini (KPLC).

Mashtaka dhidi yao yalisema kuwa makampuni yao yalikuwa yameorodheshwa kinyume cha sheria kuhusika na usafirishaji bidhaa na utoaji wa huduma kwa KPLC.

Baadhi ya wakurugenzi hawakufika kortini kama na afisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) iliomba mahakama itoe kibali cha kuwatia nguvuni.

Kiongozi wa mashtaka alimweleza hakimu mwandamizi Bw Lawrence Mugambi wa mahakama ya Milimani Nairobi kuwa washukiwa hao wamezima simu na imekuwa vigumu Polisi kuwafikia.

Bw Mugambi aliombwa atoe kibali cha kuwatia nguvuni.

Mawakili waliofika kortini kuwatetea washtakiwa walipinga ombi hilo la DPP wakisema wakurugenzi ambao hawakufika kortini walihojiwa na mkurugenzi wa idara ya jinai (DCI).

“Wakurugenzi 12 ambao hawakufika kortini walishirikiana na maafisa wa uchunguzi wa jinai waliowahoji. Hakuna haja ya kutoa kibali cha kuwatia nguvuni bila ushahidi walikataa kufika kortini,”  Bw  Mugambi alifahamishwa.

Hakimu alitupilia mbali ombi la DPP akisema “ hakuna ushahidi walikuwa wamepewa samanzi wafike kortini kujibu mashtaka na wakakataa.”

Baadhi ya wakurugenzi waliofika kortini ni pamoja na Bw Hillary Njaramba ambaye kampuni yake ya Touchline Electrical Limited ilishtakiwa kupokea Sh8,333,933 kutoka kwa KPLC.

Kampuini hiyo ilikuwa imeorodheshwa kwa njia isiyo halali kuwa itakuwa inatoa huduma za uchukuzi na huduma nyinginezo kupitia zabuni nambari KP1/9AA-02/OT/58/PJT/16-17.

Kampuni hiyo ilidai ilitoa huduma hizo kwa KPLC kati ta Aprili 12 2017 na Juni 12 2018.

Bw Njaramba ameshtakiwa pamoja na Mkurugenzi mwingine wa kampuni hiyo Bi Esther Nyambura.

Wengine walioshtakiwa ni wakurugenzi wa kampuni ya Millous Enterprises Co.Ltd Bi Catherine Wamarwa Mwangi, Catherine Wanjiku Njuguna , Christine Nyawara na Edwin Macharia Ngamini. Walikana walipokea kinyume cha sheria Sh1,413,492 kutoka kwa KPLC ilhali kampuni yao ilikuwa imeorodheshwa kwa njia isiyo halali kutoa huduma za uchukuzi na nyinginezo.

Kampuni hiyo ilipokea pesa hizo kayi ya Aprili 12 2017 na Juni 12 2018.

Washtakiwa wengine Bi Susan Wanjiru Kamau kupitia kwa kampuni yake Pestus Investments Liimited alikana alipokea Sh112,483 kutoka kwa KPLC kwa njia ya ulaghai.

Wengine waliofikishwa kizimbani Bi Catherine Wambui Mwangi, Jacquilline Wanjiru Mbaria kupitia kwa kampuni yao Kazimix Enterprises Limited wakidaiwa kupokwa Sh1,413, 492.

Kampuni ya Jake Building & Construction Limited ilishtakiwa pamoja na wakurugenzi wake Jason Morara Kerei , Jeremiah Onduko Otero, Jane Wanjiku King’ori na James Ogechi kwa kupokea Sh623,060.

Kampuni ya Gachema na wakurugennzi wake  ilishtakiwa kupkea Sh623,060. Wakurugenzi hao ni Bw Stephen Njoroge Maina, Alice Wanjiku Chege na Raphael Matheri Wanjiku.

Kampuni ya Mint Ventures Limited ilidaiwa ilipokea Sh1,702,208 .Wakurugenzi wake Petty Wanjiku Kigwe na Francis Thuku Chege walifikishwa kortini.

Kampuni nyingine ni Appenco Holdings Limited ambayo ilishtakiwa pamoja na wakurugenzi wake Mabw Samuel Gichini Njogu na Chatles Muthui Mathenge kuppkea Sh231,107.

Washtakiwa waliachiliwa kwa dhamana ya Sh400,000 pesa tasilimu.

Washukiwa 12 ambao hawakufika kortini waliagizwa wafike kortini Julai 26.

Awali hakimu alikuwa amekataa kuendelea na kesi ikiwa washtakiwa watakuwa wamejifunika nyuso kwa leso.

You can share this post!

Mzee aliyehonga jaji azirai ghafla mahakamani

Kerr mwingi wa shukrani kwa kikosi baada ya kuibuka kocha...

adminleo