• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
DPP aitisha faili ya askari jela aliyemuua mwanachuo

DPP aitisha faili ya askari jela aliyemuua mwanachuo

Na RICHARD MUNGUTI

MKURUGENZI wa Mashtaka ya Umma (DPP) ameitisha faili ya Askari jela anayeshtakiwa kwa kumgonga dafrau na kumuua mwanafunzi wa chuo kikuu katika barabara kuu ya Nairobi-Mombasa Jumapili iliyopita akiwa mlevi.

Na wakati huo huo Mahakama ya kuamua kesi za trafik ilifutilia mbali kibali cha kumtia nguvuni Konstebo Dismas Gitenge Motongwa alipochelewa  kufika kortini.

“Naomba hii mahakama isimlaumu mshtakiwa. Nilikuwa naye tukitafuta faili ya hii kesi jina lake alipoitwa lakini hakuonekana. Mnilaumu mimi mwenyewe,” wakili Danstan Omari alimweleza  hakimu mwandamizi Bi Electa Riany.

Bw Omari aliomba korti ifutulie mbali kibali cha kumtia nguvuni mshtakiwa kwa kufika kortini akiwa amechelewa.

“ Naomba korti pia imrudishie dhamana ya mshtakiwa iliyokuwa imefutiliwa mbali na mshtakiwa kuagizwa azuliwe gerezani,” Bw Omari alimsihi hakimu.

Kiongozi wa mashtaka hakupinga ombi la kufutiliwa mbali kwa kibali cha kumtia nguvunu mshtakiwa.

“Sipingi mshtakiwa akirudishiwa dhamana na pia kibali cha kumtia nguvuni kikiondolewa,” Bi Riany alifafahamishwa.

Akitoa uamuzi Bi Riany alimrudishia mshtakiwa dhamana na kumuonya vikali dhidi ya kuchelewa kufika kortini.

Mahakama iliamuru faili ya Konstebo Motongwa ipelekwe moja kwa hadi kwa DPP aisome kisha atoe ushauri.

Bi Riany alikubalia ombi la kiongozi wa mashtaka la kuahirisha kesi dhidi ya Konstebo Motongwa hadi Agosti 2 kuwezesha DPP  kusoma faili ya kesi hiyo kisha atoe ushauri jinsi kesi itakavyoendeshwa.

Mshtakiwa anakabiliwa na mashtaka matatu ya kuendesha gari akiwa mlevi, kuendesha gari bila makini na kusababisha kifo cha  Mourine Wambui Gachagua mwenye umri wa miaka 22 na kutosimama baada ya kusababisha ajali hiyo.

Mshtakiwa alikiri shtaka la kutosimama mnamo Julai 15aliposababisha  ajali kisha akatozwa faini ya Sh10,000.

Konsteno Motongwa alikuwa anaendesha garu muundo wa Volkswagen nambari ya usajili  KCN 285B mnamo Julai 15 ajali hiyo ilipotokea.

Ajali hiyo iliyotokea mwendo wa saa nane unusu karibu na duka la Nexgen Mall.

Mshtakiwa alikuwa anaelekea jijini Nairobi.

Pia anadaiwa alikuwa amekunywa pombe akapitisha kiwango  kinachokubalika dereva kuendesha gari.

Kesi dhidi ya mshtakiwa huyo itatajwa tena Agosti 2 ndipo DPP atoe mwelekeo.

  • Tags

You can share this post!

Kesi dhidi ya waziri wa kaunti aliyeaga yatupwa

Afueni kwa mabinti 22 wa UG walionaswa Kenya wakisafiri...

adminleo