• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 2:08 PM
Kesi ya Mutua kuamuliwa Agosti 6

Kesi ya Mutua kuamuliwa Agosti 6

Na RICHARD MUNGUTI

MAHAKAMA ya Juu itasikiza Agosti 6 kesi iliyowasilishwa na Gavana wa Machakos Dkt Alfred Mutua anayepinga uamuzi wa kumtimua mamlakani.

Mahakama ya rufaa ilifutilia mbali ushindi wa Dkt Mutua na kuamuru uchaguzi mdogo ufanywe katika kaunti ya Machakos.

Majaji hao walisema Dkt Mutua hakuchaguliwa kwa njia halali na kuharamisha ushindi wake.

Punde tu baada ya uchaguzi wake kubatilishwa  Gavana Mutua aliwasilisha rufaa katika Mahakama ya Juu .

Jaji Mkuu David Maraga , naibu wake Philomena Mwilu na majaji wengine watasikiza rufaa hiyo.

Ikiwa wataunga mkono uamuzi wa mahakama ya rufaa basi Dkt Mutua atakuwa Gavana wa kwanza kupoteza kiti cha ugavana baada ya uchaguzi mkuu wa Agosti 8, 2017.

You can share this post!

Afueni kwa mabinti 22 wa UG walionaswa Kenya wakisafiri...

Warembo wa Uganda wapiga magoti kumshukuru hakimu baada ya...

adminleo