• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 9:15 PM
Upatanishi wasaidia kesi 600 kutatuliwa

Upatanishi wasaidia kesi 600 kutatuliwa

Na MWANDISHI WETU

Mpango wa upatanishi uliozinduliwa na mahakama miaka miwili iliyopita, umesaidia kutatua kesi 600, Jaji Msimamizi wa Mahakama Kuu, Lydia Achode (pichani) amesema.

Alisema watu wengi wameanza kukumbatia mpango huo ambao kwa sasa umesaidia kutatua kesi hasa katika mahakama ya kututua mizozo ya kibiashara.

Akiongea katika kongamano la upatanishi la mwaka huu, Jaji Achode alisema mfumo huo unaendelea kukita mizizi katika mahakama.

Jaji Achode alisisitiza kuwa mfumo huo ni muhimu kwa kupunguza mrundiko wa kesi na kuachilia pesa zinazozimwa kwa sababu ya kesi.

Mahakama ilianza kufanyia majaribio mfumo huo Aprili 4 2016 katika mahakama ya kutatua mizozo ya kibiashara na ya kifamilia.

Baada ya mpango huo kufaulu katika vitengo hivyo, ulianza kutumiwa kutatua kesi za kijamii katika mahakama Kuu, Mahakama ya Watoto na Mahakama ya kutatua kesi za kibiashara.

Kwa sasa mipango ya kuanzisha upatanishi katika mahakama kote nchini umebuniwa na unaendelea kutekelezwa.

  • Tags

You can share this post!

NAROK: Eneo ambako ndugu huoza dada zao bila kuchukuliwa...

Mbunge afokea wanaopinga mradi wa nishati ya makaa Lamu

adminleo