• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 10:08 PM
KAWI YA JUA: KenGen yasaka ufadhili wa Sh5.7 bilioni

KAWI YA JUA: KenGen yasaka ufadhili wa Sh5.7 bilioni

Na BERNARDINE MUTANU

Kampuni ya kuzalisha umeme (KenGen) inatafuta ufadhili wa Sh5.7 bilioni kufadhili ujenzi wa kiwanda cha kuzalisha umeme kutokana na jua.

KenGen tayari imezungumza na wakopeshaji wa kimataifa ikiwemo ni pamoja na Benki Kuu ya Dunia, Benki ya French Development (AFD) na KfW, shirika la Ujerumani ambalo hufadhili miradi ya kampuni hiyo.

Ujenzi wa kiwanda cha uwezo wa megawati 45 unatarajiwa kuchukua miezi 14. Kiwanda hicho kitajengwa Embu karibu na Seven Forks Dam ambapo mradi huo utaitwa Seven Forks Solar.

Tayari uchunguzi kuhusu uwezo wa kufaulu kwa mradi huo umefanywa, alisema mkurugenzi wa maendeleo wa KenGen Moses Wekesa.

Mradi huo utazinduliwa katika kipande cha shamba cha hekta 100, Kaunti ya Embu.

You can share this post!

Kampuni ya India yaruhusiwa kuuza mbegu za GMO

Gor yahitaji Sh8 milioni kuwajibikla mechi za CAF

adminleo