Dondoo

Ajabu fundi wa nyumba akivunja ndoa ya wenyewe na kuhepa na mke wa bosi wake

Na JANET KAVUNGA August 28th, 2024 1 min read

RABAI, KILIFI

MWANADADA wa hapa alivunja ndoa yake baada ya kuzungwa akili na fundi aliyeajiriwa na mumewe kuwajengea nyumba ya kifahari.

Mume wa demu anayefanya kazi jijini Nairobi alimpa mkewe jukumu la kusimamia ujenzi pamoja na kuwalipa mafundi lakini jombi mmoja akageuka kuwa fundi wa kubomoa ndoa kwa kumnyemelea mwanadada huyo.

“Baada ya ujenzi kukamilika, jamaa aliandaa sherehe ya kuifungua na kuwaalika marafiki na watu wa familia. Hata hivyo, mkewe na fundi hawakuhudhuria sherehe hiyo na wakaenda mafichoni. Baadaye, jamaa aligundua kuwa mkewe alikuwa ameiba pesa zake na kwenda kuishi na fundi huyo mjini Mombasa,” akasema mdokezi.

Kalameni akataa kuhudhuria sherehe ya rafiki yake aliyemwalika dakika za mwisho.