Aibu yamkeketa ini mwalimu baada ya wanafunzi kumtoa mtaroni akiwa mlevi chakari
MWALIMU amekuwa gumzo eneo hili baada ya kupatikana wikendi akiwa amelala ndani ya mtaro huku amelemewa na pombe.
Inasemekana baadhi ya wanafunzi wake waliokuwa wakipita hapo walimtambua na kupigwa na mshangao.
Baada ya kusemezana kwa dakika chache walisaidiana kumtoa mtaroni wakambeba hadi pahali salama.
Tukio hilo lilisambaa haraka kupitia minong’ono ingawa lilitokea wakati wa mapumziko ya katikati ya muhula.
Baadhi ya wazazi na wakazi wamekuwa wakijadili athari za tabia ya mwalimu huyo wakipiga daruni hadhi yake kama mlezi wa wanafunzi.
Sasa wengi wanasubiri kuona jinsi atakabiliana na aibu itakayompata shuleni wanafunzi w atakaporejea kwa awamu iliyosalia ya muhula.