Buda azusha kupewa ngombe waliokonda kama mahari ya bintiye na kuagiza warudishwe
KULISHUHUDIWA kioja cha mwaka kijijini hapa baba wa msichana alipodinda kupokea ng’ombe wawili kama mahari, akidai ni dharau kwa bintiye.
Badala yake baba huyo aliamuru ng’ombe hao warudishwe walikotolewa mara moja.
Waliofika kikao hicho cha mahari walijaribu kumbembeleza akubali mifugo hao kama sehemu ya mahari, bila mafanikio kwani baba alikaa ngumu.
“Yaani wewe unanichukuliaje? Mimi nimemtunza binti yangu vyema kiasi kwamba kijana wako amependezwa naye na yuko tayari kumuoa, halafu waniletea ng’ombe mifupa mitupu? alifoka buda huyo.
“Utarudi nao. Sitachukua kamwe ng’ombe waliokonda!” akasisitiza.
Ilibidi kikao hicho cha mahari kisitishwe watu wakafumkana huku aliyeleta ng’ombe akilazimika kurudi nao.