Dondoo

Jombi adai alipapaswa na demu kwenye treni

Na THE SUN January 22nd, 2026 Kusoma ni dakika: 1

MWANAMUME mmoja amewashangaza wengi baada ya kuripoti kuwa alinyanyaswa kingono na mwanamke aliyekuwa akipita karibu na kiti chake ndani ya treni.

Kisa hicho kilitokea hadharani, jambo lililozua mjadala mpana kuhusu unyanyasaji wa kingono dhidi ya wanaume.

Polisi wametoa picha za CCTV wakimtaka mwanamke huyo ajitokeze au kusaidia katika uchunguzi. Maafisa wamesisitiza kuwa unyanyasaji wa kingono, bila kujali jinsia, ni kosa kubwa la jinai.

Wanaharakati wametoa wito kwa waathiriwa wote kuripoti visa kama hivyo bila woga.