Dondoo

Kidosho atema buda aliyekopa sukuma wiki akiwa date kwake

Na MWANDISHI WETU August 10th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

EMBAKASI, Nairobi

JAMAA mmoja alijipata pabaya baada ya mrembo wake kumtema kwa kukopa sukuma wiki kwa mama mboga.

Mdokezi anasema kalameni huyo alikuwa amemwalika demu wake nyumbani ili wazungumze na kufurahia muda pamoja.

Hata hivyo, kidosho alipofika kwenye steji, jamaa alimchukua na kuelekea naye hadi kwa kibanda cha mama mboga.

Inasemekana demu alishtuka na kukasirika alipoona jamaa akililia mama mboga amkopeshe sukuma wiki akapikie mgeni.

Kidosho alidai kitendo hicho kilimuaibisha na kumdunisha.

Alifoka: “Vipi unakopa mboga na umekuwa ukinirai nije nikutembelee? Kwani haukuwa umejipanga?” alimzomea.

Alimwambia polo kuwa hataki kuendelea kuaibishwa na mtu asiyejiandaa kwa maisha.

“Baki upangepange maisha yako kwanza,” kidosho alimwambia kabla ya kuondoka na kurejea alikokuwa ametoka.