Dondoo

Mdada afokea polo aliyemkosea heshima akimpa huduma za masaji

Na JANET KAVUNGA October 28th, 2024 Kusoma ni dakika: 1

MWANADADA mmoja alisimulia wenzake alivyotema polo aliyekuwa akimpa huduma za masaji, jamaa huyo alipomkosea heshima kwa kutamani tunda.

Mwanadada alisema alikuwa mteja wa jamaa ambaye ameajiriwa katika chumba kimoja cha kutoa huduma hizo hadi pale alipoanza kutembeza mikono yake maeneo asiyostahili na kumkosea heshima.

“Nilimfokea vikali hadi akaingiwa na woga alipoanza kunikosea heshima.”

“Tangu siku hiyo niliacha kwenda kupata huduma anakofanya kazi. Alivuka mipaka na singeweza kuvumilia,” alieleza wenzake kijiweni ambao walikubaliana naye kwamba baadhi ya watoa huduma za masaji huwa wanavuka mipaka.