Dondoo

Mrembo ashtuka kuachwa na jamaa kwa njia ya WhatsApp

Na JANET KAVUNGA September 28th, 2024 1 min read

KIPUSA mmoja mtaani hapa anajikuna kichwa akijiuliza kuhusu nini kilichomfanya mpenzi wake kumtema kupitia ujumbe wa WhatsApp siku moja baada ya kumwandalia karamu ya kukata na shoka ya kusherehekea siku yake ya kuzaliwa.

Demu alikuwa nyumbani akitazama sinema kwenye runinga, alipopokea ujumbe kutoka kwa polo akimweleza kuwa uhusiano wao ulikuwa umefikia tamati.

Kipusa alidhani jamaa alikuwa akimfanya mzaha lakini akaamini alipobaini kwamba alimbloku punde tu baada ya kumtumia ujumbe huo.

Juhudi za kumtafuta jamaa aweze kumweleza sababu ya kukatiza uhusiano wao ghafla zimegonga mwamba kwa kuwa katika ujumbe huo polo alimuonya dhidi ya kumtembelea nyumbani au kazini.