Dondoo

Wanandoa wazua drama wakizozana ndani ya baa

Na MWANDISHI WETU August 4th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

KAYOLE, Nairobi:

MAPENZI yana raha zake, lakini pia huweza kugeuka drama ndani ya sekunde chache.

Hilo ndilo lililotokea kwa wapenzi wawili waliokuwa wakichill katika baa moja katika mtaa huu kabla ya hali kubadilika ghafla na kuwa balaa.

Kwa mujibu wa wadaku, kila kitu kilikuwa sawa hadi mmoja wao alipoona ujumbe wa kutatanisha kwenye simu ya mwenzake.

Dakika chache baadaye sauti zikaanza kupanda, wote wakasimama kwa hasira huku vinywaji vikibaki mezani na wateja wengine wakipata sinema ya bure.

“Nilidhani wanataniana, lakini ghafla wakaanza kurushiana maneno makali. Baa yote ikatulia kuwatazama,” alisimulia polo mmoja.

Wapo waliosema ugomvi huo ulitokana na wivu uliokuwa umefichwa kwa muda mrefu na kuibuka baada ya ujumbe huo kuonekana.

Wafanyakazi wa baa waliwatuliza kabla ya mambo kuharibika zaidin a kila mmoja akatoka kivyake akiwa amekunja uso.