• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
Abambwa kwa kuoa msichana wa Darasa la Nne

Abambwa kwa kuoa msichana wa Darasa la Nne

Na GEORGE ODIWUOR

POLISI katika eneo la Rangwe, Kaunti ya Homa Bay wamemkamata mwanaume wa umri wa miaka 26 kwa madai ya kuishi kama mume na mke na msichana wa darasa la nne ndani ya kanisa.

Mshukiwa huyo, Okuku Okiri alikamatwa na polisi wa kituo cha Sinema AP Camp kwa ushirikiano na wanakijiji.

Mwanaume huyo alianza kuandamwa baada ya msichana huyo wa umri wa miaka 13 kukosa kuripoti shuleni kwa ajili ya muhula wa kwanza shule zilipofunguliwa mapema mwezi huu.

Inadaiwa kuwa wawili hao walikuwa wakiishi kama mke na mume ndani ya kanisa linalomilikiwa na baba ya mshukiwa.

Chifu wa eneo hilo Peter Oula alisema alipiga ripoti kwa polisi ambao walivamia kanisa hilo na kumkamata mshukiwa huyo.

“Mwanafunzi huyo aliripotiwa kutoweka wiki tatu zilizopita. Niliposikia kwamba alikuwa kanisani, niliripoti kwa polisi ili tuweze kumwokoa,” akasema chifu.

Wawili hao walipatikana ndani ya kanisa Jumamosi jioni. Mshukiwa alijitetea kuwa walikuwa wakiomba humo kanisani.

“Tunaamini kuwa wawili hao wamekuwa wakiishi pamoja tangu msichana huyo alipotoweka nyumbani,” akasema Bw Oula.

Chifu huyo alidai kuwa mshukiwa ni mwanachama wa genge la wahalifu ambao wamekuwa wakihangaisha wakazi wa eneo hilo.

Mshukiwa pamoja na baba yake, Sam Okuku na mwanafunzi huyo wanazuiliwa katika Kituo cha Polisi cha Rangwe huku maafisa wa usalama wakiendelea na uchunguzi.

  • Tags

You can share this post!

Waumini wa kanisa la Methodist wajitenga na kanisa kuu

Wabunge Mlima Kenya wasifu rais kumpa Matiang’i mamlaka

adminleo