Afisa wa itifaki wa Sakaja asaidia wasichana wawili kuingia Kidato cha Kwanza
NA SAMMY KIMATU
WASICHANA wawili werevu kutoka katika familia maskini zenye makazi Mukuru katika tarafa ya South B, Kaunti ndogo ya Starehe sasa wana furaha baada ya afisa wa itifaki wa Gavana wa Nairobi Johnson Sakaja, Bw Rodriques Lunalo, kuingilia kati kuwawezesha kujiunga na Kidato cha Kwanza.
Elizabeth Awuondo aliyefanya Mtihani wa Kitaifa wa Darasa la Nane (KCPE 2023) katika Shule ya Msingi ya St Catherine na kupata alama 371 na akapata ufadhili wake wa masomo kutoka kwa kampuni ya kuoka mikate ya Broadway mjini Thika.
