• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 11:33 PM
Akana kumeza mamilioni ya Dubai Bank

Akana kumeza mamilioni ya Dubai Bank

Na RICHARD MUNGUTI

MSHUKIWA wa wizi wa Sh159 milioni kutoka kwa benki ya Dubai aliyeamriwa Jumatano azuiliwe rumande hadi Alhamisi korti iamuru ikiwa ataachiliwa kwa dhamana au la sasa yuko huru kwa dhamana ya Sh200,000.

Hakimu mkuu Bw Francis Andayi alimwachilia  Bw Justus Lindambizi Tito kwa dhamana baada ya kuthibitisha kuwa kuna washukiwa wengine waliofikishwa mahakama awali na kuachiliwa kwa dhamana ya laki mbili.

Mahakama ilifahamishwa kuwa mnamo Ijumaa wiki iliyopita mfanyabiashata wa Mombasa Bw Zein Abubakar Said alishtakiwa kwa wizi huo na kufanya njama za kuilaghai benki hiyo.

Wakili Kirathe Wandugi anayemwakilisha Bw Tito alisema kuwa kuna kesi nyingine tatu zitakazounganishwa na hii dhidi ya  Bw Tito na Bw Said .

  • Tags

You can share this post!

#MashemejiDerby: Ingwe yalenga kuigwara Gor bila kucha za...

Wabunge wafika kortini kumliwaza mwenzao aliyeshtakiwa kwa...

adminleo