• Nairobi
  • Last Updated May 6th, 2024 1:13 PM
Aonywa asitoe habari zote kortini

Aonywa asitoe habari zote kortini

Na PHYLIS MUSASIA

MAHAKAMA ya Nakuru Jumanne ilimuonya mshukiwa wa mauaji ya ya aliyekuwa mwalimu mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kiru, dhidi ya kuzungumzia mambo yake kortini.

Jaji Joel Ngugi, alimuonya Bi Jane Muthoni, ambaye ni mjane wa marehemu Solomon Mwangi kwamba anahatarisha maisha na usalama wa wanawe.

Bi Muthoni alikuwa ameeleza korti kuhusu wakati mgumu wanaopitia wanawe akiwa gerezani.

“Nina ufahamu kwamba watoto wangu kule nyumbani wanaumia na kupitia wakati mgumu kutokana na kuzuiliwa kwangu na kutokuwepo kwa baba yao,” alieleza korti.

Alieleza kuwa wanawe wawili wanahangaika nyumbani kwa kukosa karo.

Korti iliamua mshtakiwa kupelekwa hospitali ya Nakuru Level 5 kwa matibabu maalum baada ya kudai kuwa hajaweza kupokea matibabu licha ya agizo la mahakama.

Ripoti ya daktari hapo awali ilionyesha kuwa Bi Muthoni anaugua saratani na ugonjwa wa pumu.

Kesi hiyo iliratibiwa kusikizwa Marchi 28, 29 ambapo shahidi wa mwisho atatoa maelezo yake kabla ya kesi nzima kukamilika na kusubiri uamuzi wa jaji.

  • Tags

You can share this post!

Wauguzi sasa kuajiriwa kwa kandarasi

Chelugui ajitenga na sakata ya uchimbaji mabwawa

adminleo