• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 10:50 AM
Ashtakiwa kuiba katoni 13 za mafuta ya Shell Rimula R2

Ashtakiwa kuiba katoni 13 za mafuta ya Shell Rimula R2

Na RICHARD MUNGUTI

MFANYAKAZI katika duka la kuuza bidhaa za mafuta ya petroli alifikishwa kortini kwa wizi wa katoni 13 za mafuta ya Shell Rimula R2 yenye thamani ya Sh51,385.

David Kariuki aliyefikishwa kortini akiwa amevaa surupwenye nyekundu ya kazini alikana shtaka hilo mbele ya hakimu mwandamizi Charles Mwaniki Kamau katika mahakama ya Kibera, Nairobi.

Kiongozi wa mashtaka Bw Geoffrey Obiri alimweleza hakimu, katoni hizo za mafuta ya magari zimefikishwa mahakamani kutolewa kama ushahidi ndipo zirudishwe kwa mwenyewe Bw Nites Valyi Pindoria auze.

Pia Bw Obiri alieleza mahakama hapingi mshtakiwa akiachiliwa kwa dhamana.

Bw Mwaniki alimwachilia mshtakiwa kwa dhamana ya Sh50,000.

Mahakama iliamuru ushahidi aliokamatwa nao mshtakiwa uwekwe katika stoo ya korti ndipo ukitolewa kortini mlalamishi arudishiwe.

Siku ya kusikizwa kwa kesi hiyo itatengwa Agosti 31, 2020.

  • Tags

You can share this post!

Klopp awapiku Lampard, Rodgers na Wilder kwenye tuzo za...

Beki Samuel Umtiti augua Covid-19