• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 6:39 PM
Baba kizimbani kwa kufanya ngono na bintiye

Baba kizimbani kwa kufanya ngono na bintiye

NA CECIL ODONGO

MWANAUME wa umri wa makamo Jumatano alishtakiwa katika Mahakama ya Makadara kwa kushiriki mapenzi na bintiye mwenye umri wa miaka saba katika mtaa wa Marigume, Industrial Area mjini Nairobi.

Pascal Shuga hata hivyo alikanusha mashtaka hayo mbele ya Hakimu Mkuu Mkaazi wa Makadara SPM Kithinji na kuachiliwa kwa dhamana ya Sh300,000 au mdhamini sawa na kiasi hicho huku kesi hiyo ikitarajiwa kusikizwa Machi 19.

Pascal alidaiwa alitekeleza unyama huo Jumapili Machi 3, 2019 na hakusita licha ya kilio cha uchungu wa mtoto huyo aliyesemakana alijeruhiwa vibaya katika sehemu yake nyeti.

Korti ilielezwa kuwa mkewe mshtakiwa hakuwa nyumbani wakati wa tukio na alikuwa amemwacha mwanawe nyumbani chini ya uangalizi wa mumewe pamoja na mwanawe mwengine.

Mshtakiwa aliutumia mwanya huo kumchukua mwanawe huyo na kujifungia katika chumba cha kulala aliponmtendea dhuluma hiyo kisha akamwonya vikali dhidi ya kumweleza mamake kilichojiri.

Ingawa hivyo, mtoto huyo aliyejeruhiwa vibaya baadaye alimweleza mamake kisa chote ambaye alipiga ripoti katika kituo cha polisi cha Industrial Area ambapo mshtakiwa aliandamwa na kutiwa mbaroni.

Kesi hiyo itasikizwa Juni 25, 2019.

  • Tags

You can share this post!

WHITNEY VIREGWA: Usimdharau kwa mwili wake

Jeshi latwaa uwanja wa ndege Nairobi

adminleo