• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
‘Babu Owino’ na mlinzi wake waonywa na mahakama

‘Babu Owino’ na mlinzi wake waonywa na mahakama

Mbunge wa Embakasi Mashariki, Paul Ongili almaarufu Babu Owino (kulia) na mlinzi wake Fanuel Owino wakiwa kortini Februari 5, 2018. Picha/RICHARD MUNGUTI

Na RICHARD MUNGUTI

MBUNGE wa  Embakasi Mashariki  Paul Ongili Owino almaarufu Babu Owino na mlinzi wake Fanuel Owino Jumatatu walionywa vikali kwamba wakichelewa tena kufika kortini “ wataona cha mtema kuni.”

Hakimu mwandamizi Bi Martha Mutuku aliwaonya wawili hao “watachukuliwa hatua kali endapo wataendelea kuchukulia kesi inayowakabili kimzaha.”

Hata hivyo Bi Mutuku alifutilia mbali kibali alichokuwa ametoa wawili hao watiwe nguvuni walipokosa kufika kortini wakati wa kutajwa kwa kesi inayowakabili.

Wawilli hawa wanakabiliwa na shtaka la kumpiga na kumjeruhi mlinzi katika jengo la Fortis Towers, Bw David Gichagu, eneo la Westlands Nairobi Januari 11, 2018.

Kesi dhidi yao imeorodheshwa kutajwa Feburuari 19.

  • Tags

You can share this post!

Obiri aambulia pakavu mbio za mita 3,000 Birmingham

Mahakama yaagiza polisi wasinase wakuu wa NASA

adminleo