TAIFA LEO Logo
  • Habari
    • Habari za Kitaifa
    • Habari za Kaunti
    • Kimataifa
  • Siasa
  • Maoni
  • Makala
    • Afya na Jamii
    • Lugha, Fasihi na Elimu
    • Akili Mali
    • Jamvi La Siasa
    • Shangazi Akujibu
    • Bambika
    • Pambo
    • Dimba
  • Dondoo
  • Bi Taifa
  • Mashairi
  • Michezo
  • NIE Shuleni
Habari Mseto

Chungeni msilipukiwe na gesi, Kuria aonya polisi Kiandutu

February 3rd, 2024 Kusoma ni dakika: 1
  • Shiriki mitandao ya kijamii:
  • Facebook
  • X
  • LinkedIn
  • Email
  • WhatsApp

NA MWANGI MUIRURI

WAZIRI wa Utendakazi wa Umma Moses Kuria amedai kwamba kuna kiwanda haramu cha gesi katika Kaunti ya Kiambu kinachohudumu karibu na kituo cha polisi.

Amedai kwamba kiwanda hicho alichosema kiko katika mtaa wa Kiandutu, kiko katika hatari ya kulipuka kwa wakati wowote na walio katika hatari kuu, ni maafisa wa polisi walio na afisi zao hapo karibu.

Aliongeza kwamba kituo hicho cha gesi hakina usajili wowote wa kisheria na kwamba ni haramu, ni hatari na hivyo kinafaa kuhalalishwa au kufungwa.

Soma Pia: Embakasi: Nema yatimua maafisa wanne kwa kutoa leseni tata

Wenyeji katika mtaa huo wa viunga vya mji wa Thika waliambia Taifa Leo kwamba kiwanda hicho huambatana na ukora mwingi sana hata wa kushambuliana kwa bunduki.

“Ni kiwanda cha kipekee. Mara kwa mara huwa kunazuka vita vya ufyatuliamaji risasi katika barabara ya kuingia na kutoka kiwandani humo,” akasema jirani wa kiwanda hicho.

Kiwanda cha gesi cha Kiandutu ambacho Waziri wa Utumishi wa Umma Moses Kuria amekimulika. PICHA | MWANGI MUIRURI

Hayo yanajiri huku Rais William Ruto akitoa msimamo mkali dhidi ya mamlaka za kutoa leseni kwamba wote watakaonaswa katika mtandao wa ufisadi, utepetevu na uzembe unaohatarisha maisha ya watu, watakamatwa, wafutwe kazi na kutupwa jela.

Hii ni baada ya kiwanda katika mtaa wa Embakasi kulipuka na kusababisha vifo vya watu watatu huku zaidi ya 300 wakipata majeraha.

mwangilink@gmail.com

Mfanyakazi wa Khalwale kuzikwa Jumatatu
  • Facebook
  • Twitter
  • LinkedIn
  • Email
  • WhatsApp
Maiti ya kitoto malaika yatupwa karibu na ofisi ya umma

Habari Mseto Zaidi

ODM yarudisha Kombe Magarini, Moi akitapatapa Baringo

September 12th, 2025

Upinzani wawazia kuondoa baadhi ya wawaniaji Malava kama...

September 9th, 2025

Kitendawili ahadi ya Rais Ruto kuhusu hospitali ikipuuzwa

September 1st, 2025

Patachimbika: Washirika wa Rais kugongana uchaguzi mdogo...

August 28th, 2025

Habari Za Sasa

Familia yalilia haki baada ya jamaa wao kugongwa na gari la...

September 16th, 2025

Serikali yaagizwa kubomoa daraja la wapita njia Thika Road

September 16th, 2025

KWS yaongeza ada za kuingia mbugani ikiwinda pato la Sh12...

September 16th, 2025

Wakili: Hakuna kinachomzuia Gachagua kuwania urais iwapo...

September 16th, 2025

KenyaBuzz

Freakier Friday

Years after Tess and Anna endured an identity crisis, Anna...

BUY TICKET

Weapons

When all but one child from the same class mysteriously...

BUY TICKET

The Naked Gun

Only one man has the particular set of skills... to lead...

BUY TICKET

Coffee & Contacts

Just imagine... What's the return on investment (ROI) of...

BUY TICKET

Woman Dignified Conference Season 2

Woman, Thou Art Dignified!You are cordially invited to...

BUY TICKET

Climate change from a Kenyan Perspective

Climate Change from a Kenyan Perspective: What to...

BUY TICKET
TAIFA LEO Logo

Mitandao ya kijamii

Maarufu sana

Gen-Z wa Nepal wamweka kiongozi wao madarakani

September 11th, 2025

Matiang’i pabaya? Arati kuongoza ujumbe mwingine wa Gusii kwenda Ikulu

September 11th, 2025

Ndege rasmi ya Rais kutupwa kwa kukosa ufaafu kwa matumizi ya sasa

September 14th, 2025

Usikose

Familia yalilia haki baada ya jamaa wao kugongwa na gari la polisi Eldoret

September 16th, 2025

Serikali yaagizwa kubomoa daraja la wapita njia Thika Road

September 16th, 2025

KWS yaongeza ada za kuingia mbugani ikiwinda pato la Sh12 bilioni

September 16th, 2025
Copyright © 2025 Nation Media Group. All rights reserved.