TAIFA LEO Logo
  • Habari
    • Habari za Kitaifa
    • Habari za Kaunti
    • Kimataifa
  • Siasa
  • Maoni
  • Makala
    • Afya na Jamii
    • Lugha, Fasihi na Elimu
    • Akili Mali
    • Jamvi La Siasa
    • Shangazi Akujibu
    • Bambika
    • Pambo
    • Dimba
  • Dondoo
  • Bi Taifa
  • Mashairi
  • Michezo
  • NIE Shuleni
Habari Mseto

Chungeni msilipukiwe na gesi, Kuria aonya polisi Kiandutu

February 3rd, 2024 Kusoma ni dakika: 1
  • Shiriki mitandao ya kijamii:
  • Facebook
  • X
  • LinkedIn
  • Email
  • WhatsApp

NA MWANGI MUIRURI

WAZIRI wa Utendakazi wa Umma Moses Kuria amedai kwamba kuna kiwanda haramu cha gesi katika Kaunti ya Kiambu kinachohudumu karibu na kituo cha polisi.

Amedai kwamba kiwanda hicho alichosema kiko katika mtaa wa Kiandutu, kiko katika hatari ya kulipuka kwa wakati wowote na walio katika hatari kuu, ni maafisa wa polisi walio na afisi zao hapo karibu.

Aliongeza kwamba kituo hicho cha gesi hakina usajili wowote wa kisheria na kwamba ni haramu, ni hatari na hivyo kinafaa kuhalalishwa au kufungwa.

Soma Pia: Embakasi: Nema yatimua maafisa wanne kwa kutoa leseni tata

Wenyeji katika mtaa huo wa viunga vya mji wa Thika waliambia Taifa Leo kwamba kiwanda hicho huambatana na ukora mwingi sana hata wa kushambuliana kwa bunduki.

“Ni kiwanda cha kipekee. Mara kwa mara huwa kunazuka vita vya ufyatuliamaji risasi katika barabara ya kuingia na kutoka kiwandani humo,” akasema jirani wa kiwanda hicho.

Kiwanda cha gesi cha Kiandutu ambacho Waziri wa Utumishi wa Umma Moses Kuria amekimulika. PICHA | MWANGI MUIRURI

Hayo yanajiri huku Rais William Ruto akitoa msimamo mkali dhidi ya mamlaka za kutoa leseni kwamba wote watakaonaswa katika mtandao wa ufisadi, utepetevu na uzembe unaohatarisha maisha ya watu, watakamatwa, wafutwe kazi na kutupwa jela.

Hii ni baada ya kiwanda katika mtaa wa Embakasi kulipuka na kusababisha vifo vya watu watatu huku zaidi ya 300 wakipata majeraha.

[email protected]

Mfanyakazi wa Khalwale kuzikwa Jumatatu
  • Facebook
  • Twitter
  • LinkedIn
  • Email
  • WhatsApp
Maiti ya kitoto malaika yatupwa karibu na ofisi ya umma

Habari Mseto Zaidi

Wito mtoto wa kiume pia alindwe dhidi ya maambukizi ya...

December 16th, 2025

Shakahola: Watoto walinyongwa baada ya kushinda njaa,...

December 15th, 2025

Kunguru kero tupu kwa starehe Pwani wageni wakishindwa...

December 9th, 2025

Wandayi ashutumu Kalonzo, Wamalwa kuhusu NADCO

December 7th, 2025

Habari Za Sasa

Waiguru: Ruto bado ndiye baba lao Mlima Kenya

December 22nd, 2025

Amorim adai mkosi ulichangia vijana wake Manchester United...

December 22nd, 2025

Saudi Arabia yawanyonga watu 347 mwaka huu, wengi wakiwa...

December 22nd, 2025

TAHARIRI: Tusherehekee kwa uangalifu tusije tukajuta

December 22nd, 2025

KenyaBuzz

How to Build a Library

Two intrepid Nairobi women decide to transform what used to...

BUY TICKET

Sisu: Road to Revenge

Returning to the house where his family was brutally...

BUY TICKET

The Running Man

Desperate to save his sick daughter, working-class Ben...

BUY TICKET

1ST WE BRUNCH

Step into the new year with flavour,Joy and Sparkle at our...

BUY TICKET

The Noel's Table

Gather around Noel's table for a night of warmth flavor,...

BUY TICKET

The Lady in Red

On the brink of divorce, a white woman and a black man find...

BUY TICKET
TAIFA LEO Logo

Mitandao ya kijamii

Maarufu sana

Jirongo alivyoishi maisha ya upweke

December 21st, 2025

Maafisa watatu wa Sacco washtakiwa kwa wizi wa Sh40M

December 19th, 2025

Nina mpango kabambe kwenu, Ruto aambia jamii za maeneo yaliyotengwa

December 18th, 2025

Usikose

Vicheche wa usiku walia Gen-Z kuingilia biashara yao

December 22nd, 2025

Waiguru: Ruto bado ndiye baba lao Mlima Kenya

December 22nd, 2025

Amorim adai mkosi ulichangia vijana wake Manchester United kupigwa na Aston Villa

December 22nd, 2025
Copyright © 2025 Nation Media Group. All rights reserved.