TAIFA LEO Logo
  • Habari
    • Habari za Kitaifa
    • Habari za Kaunti
    • Kimataifa
  • Siasa
  • Maoni
  • Makala
    • Afya na Jamii
    • Lugha, Fasihi na Elimu
    • Akili Mali
    • Jamvi La Siasa
    • Shangazi Akujibu
    • Bambika
    • Pambo
    • Dimba
  • Dondoo
  • Bi Taifa
  • Mashairi
  • Michezo
  • NIE Shuleni
Habari Mseto

Chungeni msilipukiwe na gesi, Kuria aonya polisi Kiandutu

February 3rd, 2024 Kusoma ni dakika: 1
  • Shiriki mitandao ya kijamii:
  • Facebook
  • X
  • LinkedIn
  • Email
  • WhatsApp

NA MWANGI MUIRURI

WAZIRI wa Utendakazi wa Umma Moses Kuria amedai kwamba kuna kiwanda haramu cha gesi katika Kaunti ya Kiambu kinachohudumu karibu na kituo cha polisi.

Amedai kwamba kiwanda hicho alichosema kiko katika mtaa wa Kiandutu, kiko katika hatari ya kulipuka kwa wakati wowote na walio katika hatari kuu, ni maafisa wa polisi walio na afisi zao hapo karibu.

Aliongeza kwamba kituo hicho cha gesi hakina usajili wowote wa kisheria na kwamba ni haramu, ni hatari na hivyo kinafaa kuhalalishwa au kufungwa.

Soma Pia: Embakasi: Nema yatimua maafisa wanne kwa kutoa leseni tata

Wenyeji katika mtaa huo wa viunga vya mji wa Thika waliambia Taifa Leo kwamba kiwanda hicho huambatana na ukora mwingi sana hata wa kushambuliana kwa bunduki.

“Ni kiwanda cha kipekee. Mara kwa mara huwa kunazuka vita vya ufyatuliamaji risasi katika barabara ya kuingia na kutoka kiwandani humo,” akasema jirani wa kiwanda hicho.

Kiwanda cha gesi cha Kiandutu ambacho Waziri wa Utumishi wa Umma Moses Kuria amekimulika. PICHA | MWANGI MUIRURI

Hayo yanajiri huku Rais William Ruto akitoa msimamo mkali dhidi ya mamlaka za kutoa leseni kwamba wote watakaonaswa katika mtandao wa ufisadi, utepetevu na uzembe unaohatarisha maisha ya watu, watakamatwa, wafutwe kazi na kutupwa jela.

Hii ni baada ya kiwanda katika mtaa wa Embakasi kulipuka na kusababisha vifo vya watu watatu huku zaidi ya 300 wakipata majeraha.

[email protected]

Mfanyakazi wa Khalwale kuzikwa Jumatatu
  • Facebook
  • Twitter
  • LinkedIn
  • Email
  • WhatsApp
Maiti ya kitoto malaika yatupwa karibu na ofisi ya umma

Habari Mseto Zaidi

Wanne wauawa wakazi wa Ikolomani wakipinga kampuni ya...

December 5th, 2025

Utata madiwani watatu sasa wakikanusha kupiga kura kubandua...

December 2nd, 2025

Rais ahimiza wanawake kujitajirisha kutokana na mipango ya...

November 28th, 2025

DCI yachunguza kifo cha mtoto katika madrassa Mombasa

November 26th, 2025

Habari Za Sasa

Mwalimu wa JS ashtaki serikali kwa kuongeza muda wa...

December 6th, 2025

Ni kuvuna: Rais Ruto alivyoingiza Trump boksi na kuvunia...

December 6th, 2025

Dhahabu ya damu: Vita vyachacha Kakamega wakazi wakipinga...

December 6th, 2025

SHANGAZI AKUJIBU: Mke hajui kupika

December 5th, 2025

KenyaBuzz

Bugonia

Two conspiracy obsessed young men kidnap the high-powered...

BUY TICKET

Regretting You

Morgan Grant and her daughter Clara explore what's left...

BUY TICKET

Springsteen: Deliver Me from Nowhere

Bruce Springsteen, a young musician on the cusp of global...

BUY TICKET

VIBE TRIBE-SAGANA EDITION

BUY TICKET

Mundoro Challenge

The Mundoro Challenge is here - A thrilling road race and...

BUY TICKET

African Women's Orchestra

Be part of the Rotary Club of Nairobi Gigiri Orchestra...

BUY TICKET
TAIFA LEO Logo

Mitandao ya kijamii

Maarufu sana

Mbinu alizotumia Ruto kumpa Gachagua funzo chaguzi ndogo

November 29th, 2025

Uasi ODM viongozi wakisusia ziara Ikulu na kulazimu Oburu kwenda peke yake

December 5th, 2025

Gachagua aangukia kitu DCP ikishinda viti 3 vya udiwani

November 29th, 2025

Usikose

Mwalimu wa JS ashtaki serikali kwa kuongeza muda wa kandarasi hadi miaka miwili

December 6th, 2025

Ni kuvuna: Rais Ruto alivyoingiza Trump boksi na kuvunia Kenya mabilioni

December 6th, 2025

Dhahabu ya damu: Vita vyachacha Kakamega wakazi wakipinga uchimbaji wa dhahabu

December 6th, 2025
Copyright © 2025 Nation Media Group. All rights reserved.