TAIFA LEO Logo
  • Habari
    • Habari za Kitaifa
    • Habari za Kaunti
    • Kimataifa
  • Siasa
  • Maoni
  • Makala
    • Afya na Jamii
    • Lugha, Fasihi na Elimu
    • Akili Mali
    • Jamvi La Siasa
    • Shangazi Akujibu
    • Bambika
    • Pambo
    • Dimba
  • Dondoo
  • Bi Taifa
  • Mashairi
  • Michezo
  • NIE Shuleni
Habari Mseto

Chungeni msilipukiwe na gesi, Kuria aonya polisi Kiandutu

February 3rd, 2024 Kusoma ni dakika: 1
  • Shiriki mitandao ya kijamii:
  • Facebook
  • X
  • LinkedIn
  • Email
  • WhatsApp

NA MWANGI MUIRURI

WAZIRI wa Utendakazi wa Umma Moses Kuria amedai kwamba kuna kiwanda haramu cha gesi katika Kaunti ya Kiambu kinachohudumu karibu na kituo cha polisi.

Amedai kwamba kiwanda hicho alichosema kiko katika mtaa wa Kiandutu, kiko katika hatari ya kulipuka kwa wakati wowote na walio katika hatari kuu, ni maafisa wa polisi walio na afisi zao hapo karibu.

Aliongeza kwamba kituo hicho cha gesi hakina usajili wowote wa kisheria na kwamba ni haramu, ni hatari na hivyo kinafaa kuhalalishwa au kufungwa.

Soma Pia: Embakasi: Nema yatimua maafisa wanne kwa kutoa leseni tata

Wenyeji katika mtaa huo wa viunga vya mji wa Thika waliambia Taifa Leo kwamba kiwanda hicho huambatana na ukora mwingi sana hata wa kushambuliana kwa bunduki.

“Ni kiwanda cha kipekee. Mara kwa mara huwa kunazuka vita vya ufyatuliamaji risasi katika barabara ya kuingia na kutoka kiwandani humo,” akasema jirani wa kiwanda hicho.

Kiwanda cha gesi cha Kiandutu ambacho Waziri wa Utumishi wa Umma Moses Kuria amekimulika. PICHA | MWANGI MUIRURI

Hayo yanajiri huku Rais William Ruto akitoa msimamo mkali dhidi ya mamlaka za kutoa leseni kwamba wote watakaonaswa katika mtandao wa ufisadi, utepetevu na uzembe unaohatarisha maisha ya watu, watakamatwa, wafutwe kazi na kutupwa jela.

Hii ni baada ya kiwanda katika mtaa wa Embakasi kulipuka na kusababisha vifo vya watu watatu huku zaidi ya 300 wakipata majeraha.

[email protected]

Mfanyakazi wa Khalwale kuzikwa Jumatatu
  • Facebook
  • Twitter
  • LinkedIn
  • Email
  • WhatsApp
Maiti ya kitoto malaika yatupwa karibu na ofisi ya umma

Habari Mseto Zaidi

Pesa za ‘Nyota’ si za kuoa, vijana waambiwa

January 14th, 2026

Gavana Nassir aajiri aliyekuwa mlinzi wa Raila kushauri...

January 8th, 2026

Utahama vyama mpaka uvimalize ila Kilifi 2027 bado ni...

December 23rd, 2025

Wito mtoto wa kiume pia alindwe dhidi ya maambukizi ya...

December 16th, 2025

Habari Za Sasa

Ida akubali uteuzi wa Ruto, asema ni heshima kubwa

January 26th, 2026

Gachagua atoroshwa, wahuni wakimvamia kanisani Othaya,...

January 25th, 2026

Murkomen: Nimeshangazwa sana na tukio la uvamizi kanisani...

January 25th, 2026

Sababu za Uhuru kupangua upya uongozi wa Jubilee

January 25th, 2026

KenyaBuzz

The SpongeBob Movie: Search for SquarePants

Desperate to be a big guy, SpongeBob sets out to prove his...

BUY TICKET

Anaconda

A group of friends facing mid-life crises head to the...

BUY TICKET

Avatar: Fire and Ash

In the wake of the devastating war against the RDA and the...

BUY TICKET

Legacy 360 Family Business Conference: Building sustainable businesses for legacy & growth

Legacy 360 Family Business conference is a one of a kind...

BUY TICKET

New Year, New Trails- Gatamaiyu Forest Reserve

Enjoy a nature trail in the Gatamaiyu Forest Reserve

BUY TICKET

RINGS & RED FLAGS!

Three couples, one apartment, and a rent deadline that...

BUY TICKET
TAIFA LEO Logo

Mitandao ya kijamii

Maarufu sana

Siasa Pwani kuchukua mkondo mpya Joho akimleta kakake Abu kwenye mwangaza

January 20th, 2026

Hofu ukabila sasa ukiteka siasa za ugavana Mombasa

January 21st, 2026

NTSA yafuta leseni za Naekana, Monna, Greenline na Uwezo sababu ya ajali

January 19th, 2026

Usikose

Ida akubali uteuzi wa Ruto, asema ni heshima kubwa

January 26th, 2026

Gachagua atoroshwa, wahuni wakimvamia kanisani Othaya, kuhutubia taifa

January 25th, 2026

Murkomen: Nimeshangazwa sana na tukio la uvamizi kanisani Witima

January 25th, 2026
Copyright © 2026 Nation Media Group. All rights reserved.