TAIFA LEO Logo
  • Habari
    • Habari za Kitaifa
    • Habari za Kaunti
    • Kimataifa
  • Siasa
  • Maoni
  • Makala
    • Afya na Jamii
    • Lugha, Fasihi na Elimu
    • Akili Mali
    • Jamvi La Siasa
    • Shangazi Akujibu
    • Bambika
    • Pambo
    • Dimba
  • Dondoo
  • Bi Taifa
  • Mashairi
  • Michezo
  • NIE Shuleni
  • ePaper
Habari Mseto

Chungeni msilipukiwe na gesi, Kuria aonya polisi Kiandutu

February 3rd, 2024 Kusoma ni dakika: 1
  • Shiriki mitandao ya kijamii:
  • Facebook
  • X
  • LinkedIn
  • Email
  • WhatsApp

NA MWANGI MUIRURI

WAZIRI wa Utendakazi wa Umma Moses Kuria amedai kwamba kuna kiwanda haramu cha gesi katika Kaunti ya Kiambu kinachohudumu karibu na kituo cha polisi.

Amedai kwamba kiwanda hicho alichosema kiko katika mtaa wa Kiandutu, kiko katika hatari ya kulipuka kwa wakati wowote na walio katika hatari kuu, ni maafisa wa polisi walio na afisi zao hapo karibu.

Aliongeza kwamba kituo hicho cha gesi hakina usajili wowote wa kisheria na kwamba ni haramu, ni hatari na hivyo kinafaa kuhalalishwa au kufungwa.

Soma Pia: Embakasi: Nema yatimua maafisa wanne kwa kutoa leseni tata

Wenyeji katika mtaa huo wa viunga vya mji wa Thika waliambia Taifa Leo kwamba kiwanda hicho huambatana na ukora mwingi sana hata wa kushambuliana kwa bunduki.

“Ni kiwanda cha kipekee. Mara kwa mara huwa kunazuka vita vya ufyatuliamaji risasi katika barabara ya kuingia na kutoka kiwandani humo,” akasema jirani wa kiwanda hicho.

Kiwanda cha gesi cha Kiandutu ambacho Waziri wa Utumishi wa Umma Moses Kuria amekimulika. PICHA | MWANGI MUIRURI

Hayo yanajiri huku Rais William Ruto akitoa msimamo mkali dhidi ya mamlaka za kutoa leseni kwamba wote watakaonaswa katika mtandao wa ufisadi, utepetevu na uzembe unaohatarisha maisha ya watu, watakamatwa, wafutwe kazi na kutupwa jela.

Hii ni baada ya kiwanda katika mtaa wa Embakasi kulipuka na kusababisha vifo vya watu watatu huku zaidi ya 300 wakipata majeraha.

mwangilink@gmail.com

Mfanyakazi wa Khalwale kuzikwa Jumatatu
  • Facebook
  • Twitter
  • LinkedIn
  • Email
  • WhatsApp
Maiti ya kitoto malaika yatupwa karibu na ofisi ya umma

Habari Mseto Zaidi

Magavana wakaliwa ngumu kuhusu hali ya kushtua ya hospitali...

May 8th, 2026

Bei ya mitumba kupanda serikali ikipendekeza ushuru mpya...

May 5th, 2026

Murkomen aagiza msako dhidi ya pombe haramu kwa kutumia...

May 4th, 2026

Familia yasaka Sh2m kuokoa jamaa anayezuiliwa na maafisa wa...

April 27th, 2026

Habari Za Sasa

Wito serikali ihakikishe watoto wote wanapata elimu bila...

May 9th, 2026

Polisi wachunguza madai shirika linahusika na ulanguzi,...

May 9th, 2026

Tshisekedi adokeza kuwania urais kwa muhula wa tatu

May 9th, 2026

Mwanasheria Mkuu atetea uteuzi wa Kindiki kuwa Naibu Rais...

May 9th, 2026

KenyaBuzz

Cats in the Museum 2: Treasures of Egypt

The main characters of the film, the mouse Maurice and the...

BUY TICKET

Brothers Under Fire

Captain Jordan Wright's squadron on leave for a wedding in...

BUY TICKET

Lee Cronin's The Mummy

The young daughter of a journalist disappears into the...

BUY TICKET

Blooms & Bond - Flower Arrangement & Vase Painting

A curated Mother's Day experience combining flower...

BUY TICKET

Fret Venture

At its core, Fret Venture has always been about...

BUY TICKET

Trivia Night

Think you're the smartest in the room? It's time to prove...

BUY TICKET
TAIFA LEO Logo

Mitandao ya kijamii

Maarufu sana

Viongozi wa Garissa waomba msamaha kwa mauaji Kitui

May 2nd, 2026

Mwisho wa ‘nganya’ wanukia korti ikipiga marufuku mapambo ya matatu

May 2nd, 2026

Gachagua alitimuliwa kuzima upinzani ndani ya serikali, mahakama yaambiwa

May 8th, 2026

Usikose

Wito serikali ihakikishe watoto wote wanapata elimu bila ubaguzi

May 9th, 2026

Polisi wachunguza madai shirika linahusika na ulanguzi, unyanyasaji wa watoto Mombasa

May 9th, 2026

Tshisekedi adokeza kuwania urais kwa muhula wa tatu

May 9th, 2026
Copyright © 2026 Nation Media Group. All rights reserved.