TAIFA LEO Logo
  • Habari
    • Habari za Kitaifa
    • Habari za Kaunti
    • Kimataifa
  • Siasa
  • Maoni
  • Makala
    • Afya na Jamii
    • Lugha, Fasihi na Elimu
    • Akili Mali
    • Jamvi La Siasa
    • Shangazi Akujibu
    • Bambika
    • Pambo
    • Dimba
  • Dondoo
  • Bi Taifa
  • Mashairi
  • Michezo
  • NIE Shuleni
Habari Mseto

Chungeni msilipukiwe na gesi, Kuria aonya polisi Kiandutu

February 3rd, 2024 Kusoma ni dakika: 1
  • Shiriki mitandao ya kijamii:
  • Facebook
  • X
  • LinkedIn
  • Email
  • WhatsApp

NA MWANGI MUIRURI

WAZIRI wa Utendakazi wa Umma Moses Kuria amedai kwamba kuna kiwanda haramu cha gesi katika Kaunti ya Kiambu kinachohudumu karibu na kituo cha polisi.

Amedai kwamba kiwanda hicho alichosema kiko katika mtaa wa Kiandutu, kiko katika hatari ya kulipuka kwa wakati wowote na walio katika hatari kuu, ni maafisa wa polisi walio na afisi zao hapo karibu.

Aliongeza kwamba kituo hicho cha gesi hakina usajili wowote wa kisheria na kwamba ni haramu, ni hatari na hivyo kinafaa kuhalalishwa au kufungwa.

Soma Pia: Embakasi: Nema yatimua maafisa wanne kwa kutoa leseni tata

Wenyeji katika mtaa huo wa viunga vya mji wa Thika waliambia Taifa Leo kwamba kiwanda hicho huambatana na ukora mwingi sana hata wa kushambuliana kwa bunduki.

“Ni kiwanda cha kipekee. Mara kwa mara huwa kunazuka vita vya ufyatuliamaji risasi katika barabara ya kuingia na kutoka kiwandani humo,” akasema jirani wa kiwanda hicho.

Kiwanda cha gesi cha Kiandutu ambacho Waziri wa Utumishi wa Umma Moses Kuria amekimulika. PICHA | MWANGI MUIRURI

Hayo yanajiri huku Rais William Ruto akitoa msimamo mkali dhidi ya mamlaka za kutoa leseni kwamba wote watakaonaswa katika mtandao wa ufisadi, utepetevu na uzembe unaohatarisha maisha ya watu, watakamatwa, wafutwe kazi na kutupwa jela.

Hii ni baada ya kiwanda katika mtaa wa Embakasi kulipuka na kusababisha vifo vya watu watatu huku zaidi ya 300 wakipata majeraha.

[email protected]

Mfanyakazi wa Khalwale kuzikwa Jumatatu
  • Facebook
  • Twitter
  • LinkedIn
  • Email
  • WhatsApp
Maiti ya kitoto malaika yatupwa karibu na ofisi ya umma

Habari Mseto Zaidi

Kijana aliyepigwa na kumwagiwa asidi na polisi hatarini...

October 27th, 2025

Stanley Kenga aamini Magarini ni kivumbi kati ya raia na...

October 13th, 2025

Wenye majengo jijini wapewa siku 14 kuyapaka rangi lau...

October 7th, 2025

Mpango wa mbolea ya bei nafuu umetekwa na wakora, EACC sasa...

October 6th, 2025

Habari Za Sasa

Kesi ya 3 yawasilishwa kupinga ujenzi wa Chuo Kikuu cha...

November 21st, 2025

Ni ahadi hewa, upinzani wamkosoa Rais

November 21st, 2025

Mpango wa harusi waishia kuwa ya mazishi

November 21st, 2025

UCHAGUZI WA 2027: Vyama vipya 25 vyasajiliwa 30...

November 21st, 2025

KenyaBuzz

Bugonia

Two conspiracy obsessed young men kidnap the high-powered...

BUY TICKET

Regretting You

Morgan Grant and her daughter Clara explore what's left...

BUY TICKET

Springsteen: Deliver Me from Nowhere

Bruce Springsteen, a young musician on the cusp of global...

BUY TICKET

VIBE TRIBE-SAGANA EDITION

BUY TICKET

Mundoro Challenge

The Mundoro Challenge is here - A thrilling road race and...

BUY TICKET

African Women's Orchestra

Be part of the Rotary Club of Nairobi Gigiri Orchestra...

BUY TICKET
TAIFA LEO Logo

Mitandao ya kijamii

Maarufu sana

Mbarire ataka Gachagua azuiwe kufanya kampeni Mbeere Kaskazini

November 17th, 2025

ODM@20: Orengo, Winnie wasema ODM haiendi kwa Ruto

November 15th, 2025

Kauli za Tutam zatanda bungeni, wabunge wakichangamkia Hotuba ya Rais Ruto

November 20th, 2025

Usikose

Kesi ya 3 yawasilishwa kupinga ujenzi wa Chuo Kikuu cha Nyamira

November 21st, 2025

Ni ahadi hewa, upinzani wamkosoa Rais

November 21st, 2025

Mpango wa harusi waishia kuwa ya mazishi

November 21st, 2025
Copyright © 2025 Nation Media Group. All rights reserved.