• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 4:55 PM
IGAD yabuni sera kurahisishia wanachama wake biashara mipakani

IGAD yabuni sera kurahisishia wanachama wake biashara mipakani

Na BERNARDINE MUTANU

JUMUIYA ya Mamlaka ya Kimataifa kuhusu Maendeleo (IGAD) imepitisha sera ya biashara isiyo rasmi nje ya mipaka pamoja na usimamizi wa pamoja wa kiusalama miongoni mwa mataifa husika.

Sera hiyo ilipitishwa Ijumaa na mawaziri kutoka mataifa husika na itawasilishwa kwa marais wa IGAD kabla ya kuwasilishwa kwa Muungano wa Afrika (AU).

Mawaziri hao kutoka Kenya, Djibouti, Ethiopia, Sudan, Sudan Kusini, Somalia na Uganda walikutana Mombasa, Kenya  walikopitisha sera hiyo.

Viongozi hao walisema sera hiyo itasaidia katika kuimarisha eneo la biashara huru Barani Afrika (FTA).

Mnamo Machi 21, zaidi ya mataifa 40 kutoka Afrika yalitia sahihi mkataba wa kuunda FTA ili kuimarisha biashara kati ya mataifa washirika.

You can share this post!

M-Tiba ya Safaricom yatambuliwa ulimwenguni

Kenya yapata mkopo mwingine kutoka Ufaransa

adminleo