• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 9:50 AM
Imam ashangaza kumlawiti mwanawe

Imam ashangaza kumlawiti mwanawe

Na Charles Lwanga

Mwalimu wa madrasa anayedaiwa kumnajisi mwanawe wa kambo mwenye umri wa miaka tisa na baadaye akampatia Sh10 na kumuonya asiseme kwa mamake, amepatikana na hatia ya kosa hilo.

Hakimu Mwandamizi wa Malindi, Bi Silvia Wewa alimuhukumu Bw Omar Said Omar, ambaye ni imamu maarufu mjini Malindi, kwa kosa analodaiwa kulifanya mnamo Machi 23, 2016.

Bi Wewa alisema upande wa mashtaka umetoa ushahidi wa kutosha unaoashiria kuwa mshtakiwa alimlawiti mtoto huyo zaidi ya mara moja.

 

  • Tags

You can share this post!

Wakuzaji miwa walia kampuni kufungwa ghafla

Safaricom yanunulia wavuvi injini za boti

adminleo