• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 9:11 AM
Jamii zilizobaguliwa kunufaika na sera ya kugawa rasilimali

Jamii zilizobaguliwa kunufaika na sera ya kugawa rasilimali

Na BERNARDINE MUTANU

Tume ya Kugawa Rasilimali (CRA) Ijumaa ilizindua sera ya pili ambayo inalenga kutambulisha maeneo yaliyobaguliwa.

Sera hiyo pia inatambulisha utaratibu wa kugawa rasilimali kutoka kwa hazina ya usawazishaji.

Kupitia kwa sera hiyo, maeneo 1424 yametambulishwa katika wadi 366, kaunti 34, kama yaliyoachwa nyuma zaidi kimaendeleo.

Sera hiyo inalenga kuimarisha upataji wa huduma za kimsingi miongoni mwa wananchi 5.6 milioni.

Baadhi ya jamii zilizotambulishwa na kuorodheshwa kuachwa nyuma kimaendeleo ni Waat, Makonde, Elmolo na Dorobo-Saletia.

Kulingana na sera hiyo, jamii hizo zinahitaji miradi maalum ili kuimarisha hali zao za kijamii na kiuchumi.

Akiongea wakati wa uzinduzi wa sera hiyo, Dkt Jane Kiringai alisema, “Tume hii ina wajibu wa kukuza sera ambayo inabainisha utaratibu wa kutambulisha maeneo yaliyoachwa nyuma kwa lengo la kugawa rasilimali kutoka kwa hazina ya usawazishaji.”

You can share this post!

Wakazi wafurahia biashara ya mafuta ndani ya Bahari Hindi

Faxe Gold, bia mpya yatua mitaani kushindana na Tusker

adminleo