• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 9:35 PM
Kesi dhidi ya waziri wa kaunti aliyeaga yatupwa

Kesi dhidi ya waziri wa kaunti aliyeaga yatupwa

Na RICHARD MUNGUTI

MKURUGENZI wa Mashtaka ya Umma (DPP) Noordin Haji amefutilia mbali kesi dhidi ya mmoja wa mawaziri wa Serikali ya kaunti ya Busia aliyeaga Bw Timon Otieno.

Otieno alishtakiwa pamoja na Gavana wa Busia Sospeter Ojaamong na mawaziri wengine watatu wa kaunti hiyo. Kesi dhidi ya Otieno iliondolewa n

Hakimu mkuu mahakama ya kuamua kesi za ufisadi (ACC) Douglas Ogoti alifahamishwa Otieno aliaga Juni 17 2018.

“Nathibitisha kuwa Timon Otieno aliaga mnamo Juni 17, 2017 . Natamatisha kesi dhidi yake,” Kiongozi wa Mashtaka Alexander Muteti alimweleza hakimu , huku akimkabidhi nakala ya cheti cha kifo cha mshtakiwa.

Bw Muteti aliwasilisha cheti kipya cha mashtaka dhidi ya Mabw Ojaamong , Bw Lenard Wanda Obimbira, Allan Ekweny Omacha na Bw Bernard Krade Yaite.

Washukiwa wengine ambao hawakufika kortini Bw Samuel Ombui, Bi Edna Adhiambo Odoyo, Renish Achieng ,Sebastian Hallensleben na Madam R Enterprises Limited watatiwa nguvuni.

Washukiwa hao hawakufika kortini na Bw Muteti aliomba watiwe nguvuni.

Na wakati huo huo mahakama ilitenga Septemba 11 siku ya kuanza kusikizwa kwa kesi dhidi ya Bw Ojaamong na wenzake watatu.

Upande wa mashtaka ulisema utachukua masaa 24 kuwasilisha ushahidi dhidi ya washtakiwa.

Bw Ogoti aliamuru upande wa mashtaka uwakabidhi washtakiwa nakala zote za ushahidi.

Pia aliamuru mawakili wanaotaka kujiondoa katika kesi hiyo wafanye hivyo mapema badala ya kung’atuka kwenye kesi siku ya kusikizwa kwa kesi na kuvurunga utaratibu.

Bw Ojaamong yuko nje kwa dhamana ya Sh1milioni pesa tasilimu.

Mahakama ilikubalia ombi la wakili Danstan Omari anayemwakilisha Ojaamong kwamba gavana huyo asiwe anaenda kupiga ripoti katika afisi za tume ya kupambana na ufisadi nchini EACC eneo la Busia kwa wafuasi wengi wa kiongozi huyo wataandamana naye.

Bw Ojaamong alikanusha shtaka la kufanya njama za kuilaghai Serikali ya kaunti ya Busia Sh8milioni kwa kuruhusu utafiti ufanywe kuhusu takataka na kampuni ya Ujeruman bila mpango.

Alikana alifanya mashauri kuhusu utoaji wa zabuni kwa kampuni ya Ujerumani bila ya kuwashirikisha maafisa wakuu wa kaunti hiyo.

Akiwa mjini Berlin, Ujerumani Gavana Ojaamong aliruhusu malipo ya Sh8milioni kinyume cha sheria.

Kesi itatajwa Septemba 4 upande wa mashtaka kueleza ikiwa umewakabidhi washtakiwa nakala za ushahidi zote.

  • Tags

You can share this post!

Bidhaa ghushi za Sh7.5 bilioni zimenaswa, walaghai 75...

DPP aitisha faili ya askari jela aliyemuua mwanachuo

adminleo