Habari Mseto

KRA yapoteza mabilioni kutokana na bidhaa ghushi

February 20th, 2018 Kusoma ni dakika: 1

Na BERNARDINE MUTANU

BIDHAA ghushi zilishusha kiwango cha mapato kutokana na ushuru kushuka kwa Sh7.35 bilioni.

Bidhaa hizo ni pamoja na stempu feki na kwa muda wa miezi sita hadi Desemba 31, zilisababisha hasara kubwa.

Kutoka Julai hadi Desemba 2017, ushuru unaotokana na uuzaji wa bidhaa ulishuka kwa asilimia tisa.

Kulingana na Shirika la Kutoza Ushuru nchini (KRA) Jumatatu, ikilinganishwa na kipindi hicho 2016 ambapo mapato kutokana na mauzo ya bidhaa yalikuwa Sh81.644, mwaka huu kiwango hicho kilishuka sana.

Katika muda wa miaka mitatu, kiwango cha mapato hayo kilikua kwa asilimia 16, alisema Kamishna Mkuu wa KRA John Njiraini.

KRA ilisema kuwa ushuru unaotakana na pombe na sigara ulishuka kwa asilimia 16.3 na asilimia 11.2 kwa mfuatano huo mwaka wa 2016.