• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 6:47 PM
M-Akiba haijafikia malengo tuliyoweka – Rotich

M-Akiba haijafikia malengo tuliyoweka – Rotich

Na BERNARDINE MUTANU

Utafiti mpya kuhusu matumizi ya M-Akiba umeonyesha kuwa huduma hiyo haifanyi vyema kama ilivyotarajiwa.

Kulingana na Waziri wa Fedha Henry Rotich, wawekezaji katika M-Akiba wanasumbuka kupata wanunuzi.

Waziri huyo alisema ili M-Akiba iweze kuimarika, lazima hati za dhamana za muda mfupi- zilizo na uwezo wa kukomaa katika muda wa chini ya miaka mitatu, kama ilivyo katika soko la rejareja.

Kutokana na hilo, Hazina ya Fedha inatathmini kugeuza mfumo M-Akiba ili kukabiliana na mahitaji katika soko la reja reja, alisema Bw Rotich Alhamisi.

Utafiti huo ulifanywa na Shirika la Financial Sector Deepening Africa likishirikiana na serikali ya Uingereza.

Mwaka 2017, ni wawekezaji 303,534 pekee ambao waliwekeza katika M-Akiba.

You can share this post!

Kundi la wenye magari kuwapa chakula wakazi wa pato la chini

M-Tiba ya Safaricom yatambuliwa ulimwenguni

adminleo